Tuesday, February 24, 2015
ZIARA YA WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA MKOANI MBEYA,IMEZUA UTATA KWA WAANDISHI WA HABARI.
Do you like this story?
Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Mbeya Wakisikiliza kwa makiini Kuhusu ujio wa Waziri Mkuu Mh Mizengo Pinda |
Na Pendo Fundisha, Mbeya.
ZIARA
ya Waziri Mkuu mizengo Pinda Mkoani
Mbeya, imezua utata kwa waandishi wa habari, kutokana na kile kinachoonekana
kuwepo kwa ubaguzi kwa vyombo vya habari
kutohusishwa katika ziara hiyo.
Utata
huo umeibuka jana, katika kikao maalum
kilichoitishwa na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya na waandishi wa habari, lengo
likiwa ni kutoa taarifa ya ujio wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, inayotarajia
kuanza kesho(leo) Mkoani Mbeya na kutembelea halmashauri saba.
Katika
kikao hicho, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbasi Kandoro, aliwafahamisha waandishi wa
habari, kwamba Waziri Mkuu Mizengo Pinda atawasili Mkoani Mbeya kesho na kwamba yupo katika ziara ya kikazi.
“Ndugu
zangu waandishi wa habari nimewaiteni hapa, kuwafahamisha kwamba Waziri Mkuu atawasili
Mbeya na kuanza ziara ya kikazi na kwamba atatembelea halmashauri saba za mkoa
wa Mbeya,”alisema Kandoro.
Hata
hivyo, baada ya Mkuu huyo, kumaliza
kutoa taarifa hiyo, baadhi ya waandishi wa habari akiwemo Mhariri Kanda za
Nyanda za Juu Kusini Kampuni ya Free Media na mwandishi mkongwe wa gazeti la
Tanzania Daima, Christopher Nyenyembe, aliomba kupatiwa utaratibu kuhusu
waandishi wa habari watakavyofanya kazi kwenye ziara hiyo.
Akitoa
utaratibu huo, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbasi Kandoro, alieleza kwamba utaratibu wa vyombo vitakavyoshiriki ziara
hiyo, umefanyika tayari kwa kutumia viongozi wa chama cha waandishi wa habari
wa Mkoa wa Mbeya.
“Ofisi
iliwasilisha taarifa kwa uongozi wa klabu na kuomba kupatiwa vyombo kumi vya
habari vitakavyoshiriki kwenye ziara hii na klabu yenu ilituwasilishia vyombo
hivyo ambavyo ni Itv, Nipashe, Tbc, Chanel Ten, Star TV, Mwananchi, Habari Leo,
Uhuru Mzalendo, Radio Bomba Fm na Mbeya FM,”alisema.
Kiongozi
huyo, alipomaliza kutoa ufafanuzi huo ndipo Mwandishi Christopher Nyenyembe
ambaye pia ni Mwenyekiti mstaafu wa Mbeya Press Club, alihoji juu ya vyombo
vingine vya habari ambavyo vimekuwa na mchango mkubwa kwa serikali hiyo ya Mkoa
lakini havimo kwenye orodha.
“Ujio
wa Pinda ni wa kitaifa, hivyo vyombe vyote vya habari vinahaki ya kupata
taarifa na kuwapasha wananchi kipi kinachoendelea lakini kwa hili
lililojitokeza hatuwezi kuitupia lawama
ofisi ya Mkuu wa Mkoa haya ni mapungufu na udhaifu mkubwa unaofanywa na
viongozi wa Press Klabu,”amesema.
Amesema,tatizo lililopo ni
kwamba klabu ya waandishi wa habari Mkoa wa Mbeya,aina mshikamano, imekuwa
ya kwanza kuwagawa wanachama hivyo kuiendesha klabu kwa urafiki zaidi hali
ambayo ni hatari kwa tasnia hii ya habari nchini huku ikipoteza lengo halisi la
uanzishwaji wa Press hizo mikoani ulioanzishwa na Baraza la habari
nchini(UTPC).
Amesema,
waandishi wa habari wamekuwa wakiitegemea klabu kama muhimili wa kuwajenga na
kuwaimarisha kitaaluma lakini hivi sasa muhimili huo umegeuka shubiri kwa
baadhi ya vyombo vya habari na waandishi wake.
“Waandishi
wanaitegemea klabu kama muhimili wa kuwajenga lakini Press hii imegeuka sehemu ya kuwabomoa
kitaaluma na kwamba endapo jambo hilo litafumbiwa macho klabu hiyo, itabaki na
watu wachache ambao hawatakuwa na nafasi ya kuwasaidia waandishi badala yake
kuangalia maslahi yao,”amesema.
Hata
hivyo, alimaliza kwa kuwataka waandishi wa habari kutoitupia lawama Ofisi ya
Mkuu wa Mkoa Mbeya, kwamba imekuwa inawabagua kwani tatizo lipo kwa viongozi wa
klabu ambao wamepewa jukumu hilo na kushindwa kuvitendea haki baadhi ya vyombo
vya habari.
Mwisho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ZIARA YA WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA MKOANI MBEYA,IMEZUA UTATA KWA WAANDISHI WA HABARI.”
Post a Comment