Tuesday, September 29, 2015
-DAWA MPYA KWA AJILI YA KUTIBU MAGONJWA YA KUHARA NA NIMONIA KUFIKA NJOMBE
Do you like this story?
Na
Gabriel Kilamlya Njombe
Viongozi mbalimbali wa ngazi ya mkoa na wilaya mkoani Njombe
wametakiwa kwenda kutumia mihadhara inayopatikana katika kutoa elimu ya
magonjwa ya Kuhara na Nimonia yanayowakumba watoto wadogo Nchini.
Kauli hiyo imetolewa na kaimu katibu tawala mkoa wa Njombe
bwana Gidion Mwinami kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wakati wa warsha ya siku
moja inayolenga kutoa elimu kwa viongozi hao na wataalamu wa afya juu ya kwenda
kuwahamasisha wahudumu wa afya katika kukabiliana na magonjwa hayo Kwa Kutumia
Dawa Mpya ya Ziora.
Kupitia Warsha hiyo Mwinami amesema anategea viongozi hao
watakwenda kuwa mabalozi wazuri wa kufikisha elimu hiyo kwa wataalamu wengine
wa afya ambao wamekuwa wakitoa huduma za magonjwa hayo kwa watoto huku akisema
takwimu zinaonesha kuwa ugonjwa wa kuhara upo kwa asilimia 32.3 ikiwa Nimonia
ni asilimia 16.3.
Kwa upande wake Dokta Rukia Ali toka wizara ya afya Amesema
wamebaini kuwepo kwa changamoto mbalimbali katika utoaji huduma ya afya kwa
watoto hao ikiwemo baadhi ya wahudumu kutokuwa na uelewa mpana namna ya
kuwahudumia watoto hao katika kukabiliana na magonjwa ya Kuhara na Nimonia.
Jackson Saitabau ni Katibu Tawala Mkoa wa Njombe Ambaye
Wakati Akifunga Warsha Hiyo Amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri Kwenda
Kuwasimamia Watumishi Wao Katika Idara ya Afya Ili Waweze Kutoa Vyema Huduma ya
Mama na Mtoto Kwa Lengo la Kupunguza Vifo Vya Watoto Chini ya Miaka Mitano.
Ufinyu wa Bajeti,Elimu duni Kwa Wataalamu wa Afya Pamoja na
Uhaba wa Dawa Kutokana na Kucheleweshwa na MSD ni Miongoni Mwa Sababu
Zilizotajwa Kukwamisha Dhamira ya Kukabiliana na Nimonia na Kuhara Kwa Watoto
Waliochini ya Umri wa Miaka Mitano Jambo Linasababisha Kuwepo Kwa Vifo Kwa
Watoto Hao Kila Mwaka.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “-DAWA MPYA KWA AJILI YA KUTIBU MAGONJWA YA KUHARA NA NIMONIA KUFIKA NJOMBE”
Post a Comment