Tuesday, September 29, 2015
AJALI YA GARI AINA YA NOAH YAUA 5 KATAVI
Do you like this story?
Watu watano wamefariki na
wengine sita kujeruhiwa katika ajali ya
gari iliyokea kijiji cha Matandalani wilaya ya
Mlele mkoani Katavi baada ya gari
aina ya NOAH lenye namba T 451 DDP
ikitokea Mpanda mjini Kuelekea Sitalike
kupinduka na kuacha njia.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari
amesema ajali hiyo imetokea majira ya
saa tano za asubuhi baada ya gari kupasuka tairi na kupinduka ambapo chanzo cha ajali kikiwa mwendo kasi.
Kaimu mganga mfawidhi wa hospitali ya wilaya ya Mpanda Daktari Teopista Elista
anasema walipokea majeruhi na miili ya
marehemu majira ya saa sita mchana
na kudai kuwa miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika hospital
hiyo Majeruhi wa ajali hiyo wanaendelea na matatibabu
na hali zao zinaendelea vizuri
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Watoto wenye miezi
tisa na miaka mitatu wamenusurika uku mama yao akipoteza maisha
Dereva wa gari hilo aliyejulikana kwa jina la Jastini Sizyindayasa anashikiliwa na polisi
Katika hatua nyingine miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika chumba cha maiti hospitali ya Mpanda uku vifaa vya kuhifadhia
Maiti vikiwa vimeharibika
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ AJALI YA GARI AINA YA NOAH YAUA 5 KATAVI”
Post a Comment