Tuesday, September 29, 2015

AJALI YA GARI AINA YA NOAH YAUA 5 KATAVI




Watu  watano  wamefariki    na  wengine  sita  kujeruhiwa  katika  ajali  ya  gari  iliyokea  kijiji  cha Matandalani  wilaya  ya Mlele  mkoani  Katavi   baada  ya  gari  aina  ya NOAH   lenye  namba  T 451 DDP  ikitokea  Mpanda  mjini  Kuelekea  Sitalike   kupinduka  na  kuacha  njia.
Kamanda  wa  Polisi  mkoa  wa  Katavi  Dhahiri  Kidavashari amesema  ajali  hiyo  imetokea  majira  ya saa tano za  asubuhi  baada  ya  gari  kupasuka  tairi  na  kupinduka  ambapo  chanzo  cha  ajali  kikiwa  mwendo  kasi.
Kaimu   mganga  mfawidhi  wa  hospitali  ya  wilaya  ya  Mpanda  Daktari  Teopista  Elista anasema  walipokea majeruhi na miili  ya marehemu  majira  ya  saa  sita mchana na kudai kuwa miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika hospital hiyo Majeruhi  wa  ajali  hiyo  wanaendelea  na  matatibabu na  hali  zao  zinaendelea vizuri
Katika  hali  isiyokuwa  ya  kawaida  Watoto  wenye  miezi tisa  na  miaka mitatu   wamenusurika  uku   mama  yao akipoteza  maisha
Dereva wa gari hilo aliyejulikana kwa jina la Jastini  Sizyindayasa  anashikiliwa  na  polisi
Katika  hatua  nyingine  miili  ya  marehemu  hao  imehifadhiwa  katika  chumba  cha  maiti  hospitali  ya  Mpanda uku  vifaa  vya  kuhifadhia Maiti  vikiwa  vimeharibika

 

0 Responses to “ AJALI YA GARI AINA YA NOAH YAUA 5 KATAVI”

Post a Comment

More to Read