Tuesday, September 29, 2015
-RAIS KIKWETE ATANGAZA HATUA 5 MUHIMU ZITAKAZOCHUKULIWA JUU YA HAKI ZA WANAWAKE.
Do you like this story?
Tanzania imeahidi
kuchukua hatua tano muhimu za kutetetea na kuendeleza haki za wanawake kati ya
sasa na mwaka 2030, ikiwa ni pamoja na kufanya mabadiliko makubwa ya kufuta
sheria zinazokandamiza wanawake na kutunga sheria za kuleta usawa wa
kijinsia,ikiwa ni utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG) mapya kwa
manufaa ya wanawake wa Tanzania.
Miongoni mwa hatua
hizo itakuwa ni pamoja na kufuta ama kufanya mabadiliko ambayo yanaendeleza
vitendo vya kiutamaduni ambavyo kwavyo vinaendeleza ubaguzi wa wanawake kama
vile Sheria ya Ndoa, Sheria ya Urithi na kutunga Sheria ya Kukomesha Ukatili
dhidi ya wanawake.
Msimamo huo wa
Tanzania umeelezwa mwishoni mwa na Rais Jakaya Kikwete wakati alipozungumza
katika Mkutano wa Usawa wa Jinsia na Uwezeshaji wa Akinamama: Dhamira ya
Kuchukua Hatua uliohudhuriwa na wakuu wa nchi mbalimbali duniani kwenye Makao
Makuu ya Umoja wa Mataifa (UN) mjini New York, Marekani.
RaisKikwete ameuambia
mkutano huo ulioitishwa kwa pamoja na Jamhuri ya Watu wa China, Denmark, Mexico
na Kenya kuwa hatua ya pili ambayo Tanzania inakusudia kuchukua ni kuridhia
makubaliano yote ya kimataifa kuhusu haki za akinamama hasa Makubaliano ya
Kimataifa Juu ya Kukomesha Aina Zote za Ubaguzi Dhidi ya Wanawake.
Hatua nyingine ambazo
Rais Kikwete amesema kuwa Tanzania itachukua katika miaka 15 ijayo ili kuhakikisha
usawa wa kijinsia nchini hatua kadhaa ikiwemo,kuendeleza na kuunga mkono
upatikanaji wa rasilimali fedha zinazolenga kuongeza usawa wa kijinsia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “-RAIS KIKWETE ATANGAZA HATUA 5 MUHIMU ZITAKAZOCHUKULIWA JUU YA HAKI ZA WANAWAKE.”
Post a Comment