Monday, September 21, 2015

DR.JOHN POMBE MAGUFULI: SITAKUA DIKTETA NITAFUATA UTAWALA WA SHERIA NITAKAPOKUWA MADARAKANI


Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo wakati akihutubia mkutano huo mjini Chato.


Mke wa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akiwasalimia wana Chato na kumuombea kura mumewe pamoja na wabunge wa CCMna Madiwani.


Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiwapigia debe wagombea ubunge wa mkoa wa Geita kutoka kulia ni Vick Kamata mgombea wa viti maalum mkoa wa Geita na Joseph Kasheku Msukuma mgombea ubunge wa jimbo la Geita vijijini.

Ali Tumbo akapanda jukwaani na Mbuzi akisakata muziki ili mradi burudani tu.

Kundi la Orijino Kemodi wakionyesha vichekesho vyao jukwaani.

Yamoto Band wakifanya vitu vyao jukwani.


Mji wa Chato na viunga vyake umetikisika huku shughuli zikisimama wakati mgombea urais wa chama cha mapinduzi Dr.John Pombe Magufuli alipokuwa akizungumza na wananchi wa mji huo na miji ya jirani.

Mgombea huyu wa kiti cha urais kupitia chama cha mapinduzi CCM ambaye pia amekuwa mbunge wa jimbo la Chato kwa miaka 20 na kulinawirisha kwa maendeleo kadhaa licha ya changamoto zilizopo amepata mapokezi yasiyo na kifani mjini Chato ambapo akizungumza na mamia kwa maelfu ya wakazi hao waliojaa katika viwanja vya shule ya sekondari Chato amewaambia watanzania endapo atapewa ridhaa ya kuwa rais wa jamhuri ya muungano amepania kuifanya Tanzania kuwa na uchumi unaotegemea viwanda na kwa kuanzia viwanda vyote vilivyobinafsishwa na kushindwa kuendelezwa na wahusika atavirejesha mikononi mwa serikali na kuvifufua.

Dr Magufuli pia amewataahadharisha wakazi wa Chato na mikoa ya kanda ya ziwa inayozungukwa na ziwa Victoria kuvua kistaarabu bila ya kutumia sumu aina ya Thiodan ili samaki waendelee kuzaliana kwa wingi na kuwanufaisha kiuchumi wakazi wanaozungukwa na ziwa Victoria na kuwaahidi kuwasaidia kwa kuwapatia ruzuku na mahitaji mengine yatakayosaidia uvuvi.

Aidha Dr Magufuli amewataka watanzania kufanya kazi kwa bidii na maarifa kwa kuwa hata katika biblia imeandkwa asiyefanya kazi na asile na kwamba jukumu lake litakuwa ni kusimamia kikamilifu na kwa uaminifu rasilimali na maliasili za nchi kwa faida ya watanzania wote na kwamba ataendesha nchi kwa kuzingatia misingi ya sheria na utawala bora.

Awali akizungumza na wakazi wa Chato kabla ya kumwalika Dr Magufuli kuzungumza na hadhira iliyokusanyika katika viwanja vya shule ya sekondari ya Chato kiongozi wa msafara wa kampeni alhaji Abdalah Bulembo amesema CCM iko tayari kwa midahalo itakayowashirikisha wagombea urais kama umoja wa katiba ya wananchi UKAWA wanavyotaka na kwamba Dr Magufuli yuko tayari wakati wowote.

0 Responses to “DR.JOHN POMBE MAGUFULI: SITAKUA DIKTETA NITAFUATA UTAWALA WA SHERIA NITAKAPOKUWA MADARAKANI”

Post a Comment

More to Read