Monday, October 12, 2015
BAADA YA MITAMBO YA MTERA KUZIMWA KIDATU NAYO YASHINDWA KUZALISHA UMEME
Do you like this story?
Baada
ya shirika la umeme nchini kuzima mitambo ya kuzalisha umeme katika kituo chake
cha Mtera, kituo kingine cha kuzalisha umeme cha Kidatu kinachotegemea maji
kutoka Bwawa la Mtera kinatarajiwa kuzima mitambo yake hivi karibuni kutokana
na kuishiwa maji kwa ajili ya kuendesha mitambo hiyo.
Meneja wa
Tanesco kituo cha kuzalisha umeme cha Kidatu muhandisi Justus Mtolela amesema
kituo hicho chenye uwezo wa kuzalisha megawati mia mbili kimepunguza uzalishaji
wake hadi kufikia megawati 30 na kwamba hali hiyo inatokana na kukosekana kwa
maji ya kuendeshea mitambo ambapo kina cha maji katika bwawa la Kidatu
kimeshuka kutoka mita za ujazo 450 hadi kufikia mita 441 huku kiwango cha
mwisho kinachoruhusiwa kuzalisha umeme kikiwa ni mita 433.
Kukauka kwa
maji katika bwawa la Mtera na Kidatu ni athari inayotokana na kukauka kwa maji
ya mto Ruaha mkuu ambao ndiyo tegemeo la bwawa hilo la Mtera linalohudumia pia
bwawa la Kidatu kwa pamoja na mto Lukosi na Iyovi ambayo na yenyewe imekauka.
Hivi karibuni
baadhi ya wataalamu na wadau wa rasilimali za maji wamekuwa na maoni na
mapendekezo kwa serikali juu ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa ili kunusuru
rasilimali hiyo na kuifanya kuwa endelevu ikiwa ni pamoja na kutazama upya
mgawanyo wa maji kwa sekta mbalimbali na pia kusimamia ufanisi katika matumizi
yake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)


0 Responses to “BAADA YA MITAMBO YA MTERA KUZIMWA KIDATU NAYO YASHINDWA KUZALISHA UMEME”
Post a Comment