Saturday, October 10, 2015
KIJANA MMOJA AFARIKI BAADA YA KUANGUKUWA NA JIWE
Do you like this story?
Kijana mmoja anayejulikana kwa jina la
Johnson Muchunguzi amefariki dunia baada ya kuangukiwa na miamba ya mawe
alipokuwa katika shughuli za uchimbaji wa mchanga kwenye eneo la machimbo
yasiyo rasmi ya Rwome yaliyopo katika kata ya Kashai Manispaa ya Bukoba,.
Baadhi ya watu walioshuhudia tukio hilo
wamesema kijana huyo pamoja na wenzake walikutwa na dhaama hiyo majira ya
asubuhi baada ya jiwe kubwa kuanguka na kumfukia wakati akiwa katika shimo
alilokuwa akichimbia mchanga.
Vikosi vya usalama pamoja na kuwahi katika
eneo la tukio havikuweza kuokoa maisha ya kijana huyo ,ambaye tayari
alikuwa keshapoteza maisha kutokana na kuzidiwa na uzito wa jiwe moja
lililomgandamiza kabla ya kufuatiwa na jiwe jingine lililokatisha tamaa juhudi
za kumuokoa zilizokuwa zikifanywa na vikosi vya usalama pamoja na wananchi.
Baadhi ya Wananchi walioshuhudia pamoja na
majirani wanaelezea kwa huzuni tukio hilo na kudai kuwa kijana huyo
alikandamizwa na jiwe kubwa ambalo lilikuwa lizito kwan walipofika eneo la
tukio walimkuta bado ni mzma akiomba msaada na kusema tukio hilo
limewahuzunisha sana.
Katika hali ya kushangaza Mwenyekiti wa
Serikali ya Mtaa wa Rwome Ponsian Wamala anakiri kuwepo kwa machimbo hayo
yasiyo rasmi,huku akishindwa kuchukua hatua zozote dhidi ya wachimbaji hao.
Hadi chanzo cha habari hii kinaondoka katika
eneo hilo bado juhudi mbalimbali zilikuwa zikiendelea kujaribu kuutoa mwili wa
marehemu Johnson kutoka katika shimo hilo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ KIJANA MMOJA AFARIKI BAADA YA KUANGUKUWA NA JIWE”
Post a Comment