|
Mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk John Pombe Magufuli
(kushoto) akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Mtama, Nape Nnauye katika
Viwanja vya soko la Majengo |
|
Mama Salma Kikwete akiwaasa wakazi wa Lindi Mjini kumchagua Magufuli kwa maendeleo. |
|
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa
Ntama (CCM) Mh. Bernard Membe akimpigia debe Magufuli Lindi Mjini katika
viwanja vya Mpilipili. |
|
Magufuli akimnadi mgombea ubunge wa Jimbo la Ruangwa, Kassim Majaliwa |
|
Magufuli na Mama Salma Kikwete wakifurahia jambo. |
Mgombea urais wa kwa tiketi ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM), John Pombe Magufuli leo 'ameibukia' katika Mkoa wa Lindi
kwa kufanya mikutano ya kampeni maeneo mbalimbali mkoani humo ikiwemo
jimbo la Mtama lililokuwa likishikiliwa na Waziri wa mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe kabla ya kumuachia Katibu wa Itikadi na
Uenezi wa CCM, Nape Nnauye anayegombea ubunge wa jimbo hilo hivi sasa.
Baadhi ya maeneo na majimbo ambayo Magufuli
alifanya kampeni hii leo ni Nachingwe katika Uwanjwa wa Sokoine huku mikutano
mingine mikubwa zaidi ya Saba akifanya katika maeneo ya Chihola, Jimbo la
Ruangwa, Jimbo la Mtama ambapo mkutano ulifanyika katika viwanja vya Soko la
Majengo.
Baada ya hapo Magufuli alimalizia kampeni
zake kwa leo katika mkutano ulihudhuliwa na umati mkubwa wa watu.
0 Responses to “MAGUFULI 'AWAIBUKIA' NAPE, MEMBE”
Post a Comment