Tuesday, October 13, 2015
WANAHABARI WATAKIWA KUFUATA MAADILI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU.
Do you like this story?
Katika
kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 25 mwaka huu wanahabari
wametakiwa kuandika habari zao kwa kufuata maadili ya uandishi wa habari ili
kuliepusha taifa na kuingia kwenye machafuko na uvunjifu wa amani.
Kauli hiyo
imetolewa na mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Ruvuma
ambaye pia ni mjumbe wa bodi ya umoja wa vyama vya waandishi wa habari
tanzania(UTPC) Bw.Andrew Kuchonjoma wakati akizungumza kwenye mkutano wa
wadau wa habari na wanahabari mjini Songea mkutano uliobeba agenda ya
wanahabari na uchaguzi.
Kwa upande wake
mmoja wadau wa habari mkoani Ruvuma ambaye alimwakilisha mkuu wa mkoa wa Ruvuma
kwenye mkutano huo Bw. Frolence Kundi amesema habari ni kitu muhimu katika
jamii na kwamba wanahabari mkoani ruvuma wamekuwa na mchango mkubwa katika
kuripoti masuala ya uchaguzi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WANAHABARI WATAKIWA KUFUATA MAADILI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU.”
Post a Comment