Thursday, October 29, 2015
SUGU AZUNGUMZA JINSI CHADEMA ITAKAVYOFANYA KAZI MBEYA.
Do you like this story?
Mbunge mteule
wa Jimbo la Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amesema chama hicho
kitahakikisha kinampata meya mpya mwenye uwezo wa kusimamia miradi ya maendeleo
inayopangwa kila mwaka.
Sugu aliyasema
hayo jana, wakati akizungumzia mikakati ya Chadema baada ya kupata ushindi
katika kata 26 kati ya 30 za jimbo lake.
“Tutamchagua
meya atakayezuia mianya yote ya rushwa na uonevu pamoja na kusimamia sheria
rafiki na siyo kandamizi,” alisema Sugu.
Alisema Mbeya
itakuwa mfano wa kuigwa na majiji mengine ndani na nje ya nchi kutokana na
mpangilio utakavyokuwa katika kutatua kero ambazo zilikuwa kikwazo kikubwa cha
maendeleo kwa wananchi.
Diwani mteule
wa Kata ya Isanga, Anyandwile Mwalwiba, alisema wamejipanga kumpata meya
atakayekuwa tayari kuendana na kasi kubwa ya maendeleo na kulibadilisha Jiji la
Mbeya.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SUGU AZUNGUMZA JINSI CHADEMA ITAKAVYOFANYA KAZI MBEYA.”
Post a Comment