Friday, January 22, 2016
DKT KIKWETE ATUNUKIWA SHAHADA YA HESHIMA YA MAHUSIANO YA KIMATAIFA OUT.
Do you like this story?
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania Dkt Asha Rose Migiro akifungua rasmi mahafali ya 30 ya Chuo Kikuu Huria Tanzania yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam. |
Rais mstaafu wa awamu ya nne Mhe Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wanataaluma na wageni katika maafali ya 30 ya Chuo kikuu Huria Tanzania yaliyofanyika Jijini Dare s Salaam. |
Baadhi ya wahitimu wa shahada mbalimbali kutoka Chuo kikuu Huria Tanzania. (Picha zote na Raymond Mushumbusi Maelezo)
|
Na Raymond Mushumbusi Maelezo
Rais mstaafu wa awamu ya nne Mhe Dkt Jakaya Mrisho
Kikwete ametunukiwa Shahada ya heshima ya udaktari wa falsafa wa mahusiano ya
kimataifa Jijini Dar es Salaam katika mahafaliya 30 ya Chuo Kikuu Huria
Tanzania.
Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amesema amefarijika
sana kutunukiwa shahada hiyo ya heshima itolewayo na Chuo kikuu Huria Tanzania
kwa watu ambao wametoa mchango katika maendeleo katika jamii kupitia nafasi zao
kiutendaji.
“Naipokea heshima hii toka Chuo Kikuu Huria Tanzania
kwa moyo mmoja kwani wameona mchango ambao nimeutoa nilipokuwa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania kwa Awamu ya Nne hivyo basi nitaendeleza mahusiano na
ushirikiano kimataifa”.Alisema Mhe. Dkt Kikwete.
Mbali na Dkt Jakaya Mrisho Kikwete kuna baadhi ya
maraisi na wakuu mbalimbali duniani waliwahi kupata Shahada za heshima toka
Chuo Kikuu Huria Tanzania ambao ni Rais wa Awamu ya kwanza wa Tanzania Mwalimu
Julius Kambarage Nyerere, Rais wa Awamu ya pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi, Rais
wa Awamu ya tatu Benjamin William Mkapa, Rais wa zamani wa Afrika ya Kusini
Hayati Nelson Mandela na Dkt Koichiro Mastuura Mkurugenz iwa UNESCO.
Chuo kikuu Huria cha Tanzania kimetoa jumla ya
wahitimu 69 wawili Shahada maalum na 67 ni Shahada, Stahahada na Astashahada,
ambapo Shahada ya uzamivu ni wahitimu watatu, Shahada ya uzamili ni wahitimu
20, Shahada wahitimu 22,Stashahada wahitimu 15 na Astashahada wahitimu 6.
Tangu kuanzishwa kwa Chuo Kikuu Huria Tanzania mwaka
1992 jumla ya wahitimu 25,908 wametunukiwa Shahada mbalimbali na haya ni
mahafali ya 30 tangu chuo kuanzishwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ DKT KIKWETE ATUNUKIWA SHAHADA YA HESHIMA YA MAHUSIANO YA KIMATAIFA OUT.”
Post a Comment