Friday, January 22, 2016
KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE ZATANGAZWA
Do you like this story?
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Job Ndugai ametangaza kamati za Bunge na majina ya wabunge
waliochaguliwa katika kamati hizo kwa mujibu wa sheria.
Sura za wabunge wa zamani zimechanganyika na
sura mpya katika kamati hizo ambapo Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe (ACT) na
Mbunge wa Ubungo Saed Kubenea (CHADEMA) ni miongoni mwa wanaounda kamati ya
huduma za maendeleo ya jamii.
Mbunge wa Nyamagana Stanslaus Mabula (CCM),
Naghejwa Kaboyoka Same mashariki (CHADEMA)Livingstone Lusinde Mtera (CCM)
wameteuliwa kujumuika katika kamati ya Hesabu za serikali PAC.
Kamati nyingine ni pamoja na Kamati ya
Uongozozi ikiwa na Spika Job Ndugai ambaye ni Mbunge wa Kongwa (CCM), Freeman
Mbowe Hai (CHADEMA) George Masaju ambaye ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na
wengineo.
Kamati ya sheria ndogo waliopata nafasi ni
pamoja na Halima Mdee Kawe (CHADEMA),Abdalah Mtolea Temeke (CUF) ,Tundu Lissu
Singida Mashariki (CHADEMA),Ridhiwani Kikwete Chalinze (CCM).
Baadhi ya wanaounda kamati ya Serikali za
mitaa ni pamoja na Kangi Lugola Mwibara (CCM) Leah Komanya Viti maalum (CCM)
Saada Mkuya Welezo (CCM) na wengineo.
Aidha Spika wa Bunge amesema kuwa kamati hizo
zimeundwa kwa kuzingatia uzoefu wa wabunge hao,taaluma zao na jinsi walivyojaza
fomu za kuomba kamati hii
MAJINA YA KAMATIO ZOTE SOMA HAPA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE ZATANGAZWA ”
Post a Comment