Thursday, January 21, 2016
WAMILIKI WA SHULE, VYUO BINAFSI WAMPONGEZA NDALICHAKO.
Do you like this story?
Mwenyekiti Taifa wa Shirikisho la Shule na Vyuo Visivyo vya Serikali, Mrinde Mnzava (kulia) akitoa ufafanuzi kwa wanahabari |
WAMILIKI wa shule na vyuo binafsi kupitia
Shirikisho la Wamiliki wa Shule na Vyuo Visivyo vya Serikali wamempongeza
Waziri wa Elimu, Sayansi,Teknolojia na Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako kwa
kuliagiza Baraza la Taifa la Mitihani kufanya mapitio ya mfumo unaotumika wa
sasa wa wastani wa alama (GPA) na kurudisha katika mfumo wake wa zamani wa
‘division’.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es
Salaam, Mwenyekiti Taifa wa Shirikisho hilo (TAMONGSCO), Mrinde Mnzava, amesema
kuwa kupitia shirikisho lao wanampongeza waziri huyo kwa kutoa ufafanuzi juu ya
alama za mtihani zilizokuwa zikitumika kwa wanafunzi katika matokeo yao ya
mitihani ya sekondari ambapo alama hizo zilikuwa zikileta sintofahamu kwa
wazazi walio wengi hapa nchini.
Amesema agizo lake la kuliagiza Baraza la
Taifa la Mitihani kupitia mfumo wake upya uliokuwa ukitumika wa GPA ni kwamba
sasa wazazi waliokuwa wakienda shuleni kufafanuliwa matokeo ya watoto wao juu
ya ufaulu wataweza kufurahia mfumo wa zamani uliokuwa ukitumika wa ‘division’.
Alifafanua kuwa mfumo huo wa GPA ulikuwa
unashusha kiwango cha elimu ambapo mwanafunzi alionekana kupata wastani mzuri
hata kama alikuwa amefeli kwa kuonesha amefaulu katika alama za chini tofauti
na mfumo wa zamani.
Mrinde alieleza kuwa kupitia shirikisho lao
watahakikisha wanafunzi wanaendelea kupata elimu bora kwani sababu kubwa
zinazopelekea wanafunzi kufeli ni kutokana na kuyumbishwa kwa kubadilisha
mitaala ya elimu.
Akizungumzia viwango vya ada wanazotoza
katika shule zao alisema wanasubiri kupewa waraka elekezi wa viwango husika na
hawana sababu ya kupingana na serikali kwani hata serikali haiwezi kushusha
viwango vya ada kuwa chini kabisa bila kuangalia huduma zinazotolewa na shule
hizo.
(NA DENIS MTIMA/GPL)
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ WAMILIKI WA SHULE, VYUO BINAFSI WAMPONGEZA NDALICHAKO.”
Post a Comment