Thursday, March 10, 2016
RIPOTI YA MADAWA YA KULEVYA YAZINDULIWA NCHINI, BIASHARA YA BANGI, MIRUNGI, HEROIN YAONGOZA.
Do you like this story?
Uzinduzi wa Ripoti ya Bodi ya Kimataifa ya Kuzuia Madawa ya Kulevya (INCB) ukifanyika. |
Mkuu wa Elimu, Habari na Takwimu kutoka Tume ya Taifa ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Amani Msami akisoma ripoti ya Bodi ya Kimataifa ya Kuzuia Madawa ya Kulevya (INCB). |
Kituo cha Habari cha
Umoja wa Mataifa (UNIC) kimezindua ripoti ya Bodi ya Kimataifa ya Kuzuia Madawa
ya Kulevya (INCB) na kuelezea hali ya matumizi ya madawa ya kulevya ilivyo
nchini na hatua zinazotakiwa kuchukuliwa.
Akisoma ripoti hiyo,
Mkuu wa Elimu, Habari na Takwimu kutoka Tume ya Taifa ya Kudhibiti Dawa za
Kulevya, Amani Msami alisema katika ripoti hiyo inaonyesha kuanzia mwaka 2014
biashara ya Bangi, Mirungi na madawa ya kulevya aina ya Heroin yaliongezeka na
katika kipindi cha mwaka 2013 zaidi ya Kilo 321 za Heroin zilikamatwa nchini.
Alisema nchi za
Afrika Mashariki zimekuwa zikitumika kama sehemu ya kupitishia madawa kwenda
maeneo mengine ya dunia ambapo dawa hizo zimekuwa zikitokea nchi za Afghanstan,
India, Iran na Pakistan na kupelekwa nchi kama China, Japan, Afrika Kusini,
Marekani na nchi zingine za Ulaya.
Aliongeza kuwa madawa
hayo yamekuwa yakipitishwa nchini kwa kutumia meli kubwa ambazo zimekuwa
zikitumia majahazi, mashua, ngalawa na boti ziendazo kasi ili kufikisha madawa
ya kulevya nchi kavu.
Aidha alieleza
kupitia ripoti hiyo inaonyesha kuwa katika kila watu 100 barani Afrika, watu 8
wanakuwa wanatumia bangi na hivyo kuifanya bangi kuongoza kwa matumizi makubwa
Afrika na zaidi matumizi ya bangi ipo nchi za Afrika Magharibi na Afrika ya
Kati.
Madawa mengine
yanayoongoza kwa matumizi makubwa Afrika ni pamoja na madawa aina ya Heroin
ambapo katika watu 1,000 watu 3 wanatumia madawa hiyo na Cocaine inashika
nafasi ya tatu kwa matumizi makubwa.
Pia alisema kuwa ripoti
imezitaja nchi za Tanzania, Kenya na Senegal kwa kuanza kutoa huduma ya kuwapa
waathirika wa matumizi ya dawa za kulevya, dawa za Methadone ambazo zinasaidia
kuwarudisha waathirika katika hali zao za awali.
“Ripoti hii
inaonyesha jinsi hali ilivyo na Tanzania kama nchi wanachama inatakiwa ifanye
baadhi ya marekebisho ili kuzuia biashara na matumizi na hawa wafanya biashara
wa haya madawa wanatumia sana watu wenye kipato cha chini na wakifikisha mizigo
yao wanawalipa,” alisema Msami.
Nae Afisa wa Umoja wa
Mipango wa Umoja wa Mataifa anayesimamia udhibiti wa dawa za kulevya na uhalifu
unaosababishwa na madawa ya kulevya, Immaculate Maliyamkono alisema ripoti
imeyotolewa na INCB inaonyesha kuwa bado kuna biashara ya madawa za kulevya kwa
nchi za Afrika Mashariki na hivyo ni wajibu wao kama wanachama wa bodi hiyo
kuangalia upya sera zao ili kudhibiti biashara na matumizi ya madawa ya
kulevya.
“Kama ripoti
imevyoonyesha INCB inawataka wanachama wake wafanye sawa na mkataba wa mwaka
2009 ili kuzuia biashara ya haya madawa na hatua zinazoweza kuchukuliwa ni
pamoja na kubadili sera inayotumika sasa,” alisema Bi. Maliyamkono.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “RIPOTI YA MADAWA YA KULEVYA YAZINDULIWA NCHINI, BIASHARA YA BANGI, MIRUNGI, HEROIN YAONGOZA.”
Post a Comment