Wednesday, June 8, 2016
AMOSI MAKALLA: BARABARA ZOTE ZILIZO CHINI YA KIWANGO ZIRUDIWE MARA MOJA. MBEYA
Do you like this story?
Mkandarasi akiwa katika eneo la kazi Kuziba Sehemu ambazo Zimeharibika. |
Mwananchi akitoa kero zake kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh Amosi Makalla mara Baada ya kufanya Ziara ya kukagua Barabara zilizojengwa na Mradi wa Bank ya Dunia.(Picha na David Nyembe wa Fahari News) |
Mkuu
wa mkoa wa Mbeya Amos Makala ameuagiza uongozi wa jiji la Mbeya kuhakikisha
wanasimamia ukarabati wa barabara zote za jiji zinazodaiwa kujengwa chini ya
kiwango.
Makalla
amesema hayo wakati wa ziara yake ya kutembelea na kukagua barabara kadhaa
jijini hapa zilizojengwa na serikali kupitia mradi ya banki ya dunia.
Amesema
barabara hizo zinatakiwa kurudiwa kwa kiwango cha ubora kwa kile alichoeleza
kuwa barabara hizo zimegharimu kiasi cha fedha zaidi y ash.bilioni 23 ambapo
amewataka pia madiwani wa halimashauri ya jiji kuhakikisha wanasimamia fedha
zinazotolewa na serikali kwa ajili ya shughuli za maendeleo.
Hata
hivyo mhandisi wa barabara jiji la mbeya Oswald Kasambala amekiri kuwepo kwa
tatizo hilo na kuahidi kukarabati barabara hizo upya na kwamba miongoni mwa
sababu za kuharibika barabara hizo ni magari yenye uzito mkubwa kutumia
barabara hizo ambazo tayari zimeanza kufanyiwa maboresho ikiwa ni pamoja na
upanuzi wa mitaro ya maji
Baadhi
ya wananchi waliopata fursa ya kutoa malalamiko yao kwa mkuu wa mkoa wamedai
kuwepo kwa kero ya maji kujaa hususani nyakati za mvua hivyo kuiomba serikali
kuhakikisha barabara zinazojengwa zinakidhi matakwa ya jamii.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “AMOSI MAKALLA: BARABARA ZOTE ZILIZO CHINI YA KIWANGO ZIRUDIWE MARA MOJA. MBEYA”
Post a Comment