Saturday, June 11, 2016
VIDEO: UFARANSA YAANZA VYEMA MASHINDANO YA EURO 2016
Do you like this story?
Wenyeji wa mashindano ya EURO 2016, Ufaransa
wamefungua mashindano hayo kwa kuibuka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya
Romania, mchezo ulioshuhudiwa na mashabiki 75,113 katika dimba la Stade de
France lililopo katika jiji la Paris.
Ushindi wa Ufaransa ulipatikana kupitia mshambuliaji
Olivier Giroud katika dakika ya 57 baada ya kuunganisha kwa kichwa mpira mrefu
uliopigwa na Dimitri Payet na Payet mwenyewe kufunga goli la pili na la ushindi
katika dakika ya 89 baada ya kupiga shuti kali lililomshinda goli kipa wa
Romania, Ciprian Tatarusanu.
Goli pekee la Romania katika mchezo huo lilifungwa
na Bogdan Stancu kwa njia ya penati baada ya beki wa Ufaransa, Patrice Evra
kumchezea faulo mchezaji wa Romania, Stanciu.
Kwa matokeo hayo, Ufaransa imekuwa kinara wa kundi A
ikiwa na alama tatu na Romania ikishika mkia wa kundi hilo.
Michezo inayotaraji kuchezwa leo Jumamosi ni,
Albania na Switzerland majira ya saa 16:00 jioni, Wales na Slovakia saa 19:00
usiku na England na Urusi saa 22:00 usiku.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ VIDEO: UFARANSA YAANZA VYEMA MASHINDANO YA EURO 2016”
Post a Comment