Monday, November 7, 2016
CRISTIANO RONALDO KUSAINI MKATABA MPYA REAL MADRID HADI 2021
Do you like this story?
Klabu
ya Real Madrid imetangaza rasmi kuwa nyota wao Cristiano Ronaldo, November
7/11/2016 jumatatu atasaini kandarasi mpya itakayomfanya aitumikie timu hiyo
mpaka mwaka 2021 (atakuwa na umri wa miaka 36).
Kazi kubwa iliyofanywa na rais Florentino Perez, ambaye kwa kiasi
kikubwa alichukua jukumu la kuzungumza na nahodha huyo wa timu ya taifa ya
Ureno.
“Ronaldo atasaini mkataba mpya baadae hii leo, na kisha
atazungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano Santiago Bernabeu
stadium kuanzia saa saba na nusu mchana” imeeleza taarifa iliyotolewa na Real
Madrid.
“Mshambuliaji huyo kutoka nchini Ureno atasaini mkataba ambao
utamuweka hapa hadi Juni 30-2021, atakua sambamba na rais wa klabu Florentino
Perez, katika mkutano na waandishi wa habari.” Imeongeza taarifa hiyo
Ronaldo anakua mchezaji wa pili kukubali kusaini mkataba wa
kuendelea kuitumikia Real Madrid, akitanguliwa na Gareth Bale ambaye alifanya
hivyo juma lililopita.
Ronaldo mwenye umri wa miaka 31, alijiunga na Real Madrid akitokea
Manchester United kwa ada ya uhamisho ya Pauni milioni 80 ambayo iliweka rekodi
ya dunia kwa mwaka 2009.
Mpaka sasa ameshaifungia klabu hiyo mabao 350, sambamba na kutwaa
ubingwa wa Ulaya mara mbili, ubingwa wa ligi ya Hispania mara mbili, ubingwa wa
kombe la Mfalme mara mbili, Supercopa mara mbili, UEFA Super Cup na klabu
bingwa duniani (FIFA Club World Cup) mara moja.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “CRISTIANO RONALDO KUSAINI MKATABA MPYA REAL MADRID HADI 2021”
Post a Comment