Saturday, April 22, 2017

Afariki Dunia kwa kutumbukia kisimani


Mtu mmoja ambae ni mgonjwa wa akili amefariki Dunia baada ya kutumbukia ndani ya kisima  kilichopo maeneo ya Sokoni mzuri Makunduchi.
Kwa mujibu wa taarifa zilizosibitiswa na kaimu kamanda wa Mkoa wa Kusini Unguja, Kamishna Msaidizi wa Polisi Kheri Mussa kuwa marehe huyo aliyejulika kwa jina la Wanu Ameir Chum ambapo tukio hilo limetokea jana huko Mzuri Makunduchi.
Aidha Kamanda huyo alitoa wito wa watu wanaoishi na wagonjwa wa akili kuwa karibu nao na kutowaacha peke yao majumbani ili kuweza kuepusha majanga kama hayo.
Mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi katika Hospitali ya Koteji Makunduchi na kukabidhiwa kwa jamaa zake kwa ajili ya mazishi.

0 Responses to “Afariki Dunia kwa kutumbukia kisimani ”

Post a Comment

More to Read