Thursday, March 20, 2014
POLISI MBEZI WADAIWA KUUMA FUNDI UJENZI.
Do you like this story?
Kamanda wa polisi mkoa wa kinondoni camilius
wambura
|
Polisi wa kituo cha
Mbezi kwa yusuph jijini dar es salaam,
wanadaiiwa kumuua kwa kumpiga fundi ujenzi aliyetajwa kwa jna la elinema massawe.
Binamu wa marehemu,
Gilbeth mushi amesema jana kuwa kifo cha
ndugu yake kimetokana na kipigo alichopata kutoka kwa askari wa kituo hicho
ingawa polisi mkoa wa kinondoni imesema
inachunguza suala hilo.
Walimkamata ijumaa
iliopita akiwa mzima kwenye
shughuli zake za ujenzi mbezi.
Walimhuisha na tukio la wizi wa gari, wakampeleka kituoni alipopigwa vikali sehemu
mbalimbali mwilini amesema binamu.
Walimvunja miguu kutokana
na kipigo, mke wake aliwaomba wamruhusu akatibiwe lakini askari
walimkamata mpaka juzi walipoona hali yake mbaya ndipo
wakamruhusu akiwa chini ya ulinzi.
Mushi amesema ndugu yake
alifariki dunia kabla ya kuanza kupewa matibabu katika hospitali ya tumbi, kibaha na sababu kubwa ni kupoteza damu nyingi kutokana na majeraha aliyoyapata.
Imeniuma sana askari tuliyekwenda naye hospitali alidanganya kwa
muuguzi kwa kusema marehemu alikuwa kwenye hali mbaya kutokana na kipigo kutoka kwa wananchi, alisme mushi.
Kamanda wa polisi mkoa wa
kinondoni camilius wambura amesema taarifa
kuhusiana na kifo cha elinema amezipata .
Suala la kufa mtu lazima
liangaliwe kwa makini ili kujua sababu za kweli za kifo. Tunataka kujua wapi
alipokamatwa na katika mazingira
gani.
Tunaendelea kuchunguza kwa
kina kasha tunatoa taarifa alisema wambura.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “POLISI MBEZI WADAIWA KUUMA FUNDI UJENZI.”
Post a Comment