Thursday, March 20, 2014
MTUHUMIWA DAWA ZA KULEVYA ATOA KETE 82.
Do you like this story?
Kitengo cha kudhibiti dawa
za kulevya nchini kimesema
mtuhumiwa mashusha matata hadi sasa ameshatoa kete 82 za dawa
ya kulevya aina cocaine zenye thamani y ash 83.6 millioni.
Matata alikamatwa machi
17 mwaka huu, saa 8 mchana katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius nyerere akitoka brazil alitua na ndege ya shirika la ndege la
Ethiopia.
Akizungumza jana kamanda
wa kitengo hicho godfredy nzowa alisema awali mtuhumiwa alitoa kete 21 kwa njia ya haja kubwa.
Kamanda nzowa amesema matata alitoa kete hizo kwa awamu tatu kwanza kete 30 baadaye kete 31 siku inayofuata alitoa kete 21.
Amesema mtuhumiwa huyo
akiwa na hati ya kusafiria yenye namba AB362172
mali ya Tanzania alitiliwa shaka na askari polisi hivyo kumtia nguvuni.
Aliposhuka uwanja wa ndege
tulimshuku huenda akawa amebeba dawa za kulevya. Tuliamua kumhoji kabla ya kuja
kukubali saa moja baadaye amesema nzowa.
Kamanda nzowa amesema bado
wanaendelea na upelelezi na kwamba hatua hiyo itakapo kamilka atasomewa
mashataka mahakama kuu kwa vile thamani ya dawa hizo ni kubwa na mtuhumiwa bado anaendelea
kuzitoa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MTUHUMIWA DAWA ZA KULEVYA ATOA KETE 82.”
Post a Comment