Thursday, March 20, 2014
SULUHU: NITAFUATA NYAYO ZA ATTAH MILLS.
Do you like this story?
Makamu mwenyekiti wa bunge la katiba samia suluhu Hassan. |
Makamu mwenyekiti wa bunge
la katiba samia suluhu Hassan amesema atatumia mtindo wa aliyekuwa Rais wa Ghana hayati Profesa John Attah Mills kwenye
mijadala ya kuboresha rasimu za katiba bungeni ili kujiandalia mazingira mazuri
ya maisha yake ya baadaye.
Kauli hiyo inalenga kuunga
mkoni jitihada za wawakilishi wa jumuiya wa wazee Tanzania waliofika ofisini kwake bungeni kuwasilisha
maombi yao ya kutaka wabunge kuzingatia
haki zao wakati wakitelekeza majukumu hayo .
Msafara wa wazee hao
ulliongozwa na mwenyekiti wa jumuiya
hiyo Sebastian bulega na katibu wa jumuiya ya wastaafu na wazee Zanzibar , DK
yusuf Nuh Pandu uliomba katiba ijayo
itoe tafsiri ya mzee kuwa ni mwanamke au mwanaume mwenye umri wa mika a kuanzia
60.
Bulega lisema wanataka
ibara ya 10(iv) iliyo kwenye rasimu
ibakizwe na ili itekelezwe vizuri walitaka tafsiri ya mzee kwa maana ya
umri iainishwe . ibara hiyo ipo kwenye sura
ya pili inayohusu malengo, misingi ya mwelekeo wa shughuli za serikali na sra za kimataifa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SULUHU: NITAFUATA NYAYO ZA ATTAH MILLS.”
Post a Comment