Thursday, March 20, 2014
SERIKALI KUHAMIA DODOMA KESHO.
Do you like this story?
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika
picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mh.Samuel
Sitta(kushoto) na Makamu Mwenyekiti Mhe.Samia Suluhu(kulia).
|
UONGOZI
wa juu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar (SMZ), kesho utahamia katika Makao Makuu ya Tanzania, Dodoma,
kushuhudia hotuba ya kihistoria itakayotolewa na Rais Jakaya Kikwete mbele ya
Bunge Maalumu la Katiba.
Hotuba
hiyo ya Rais inasubiriwa kwa hamu na Watanzania, kutoa dira kwa wajumbe wa
Bunge hilo
Maalumu
la Katiba, wakati watakapokuwa wakiandika Katiba mpya.
Mmoja wa wajumbe wa Bunge hilo, ambaye ni mmoja wa wanasiasa wakongwe, aliliambia gazeti hili kuwa anatarajia hotuba ya Rais Kikwete itakuwa ya kujenga Bunge na sio kubomoa kwa kuzungumzia misimamo ya vyama.
“Yeye
ni kiongozi wa Taifa, hivyo natarajia atakuja hapa kutupa njia na namna ya
kushughulikia changamoto zilizopo wakati tunapoenda kuandika Katiba mpya,”
alisema mwanasiasa huyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.
Akizungumza
jana na waandishi wa habari Katibu wa Bunge Maalumu la Katiba, Yahya Khamis
Hamad alisema Rais atahutubia Bunge saa 10 jioni na wageni waalikwa watatakiwa
kuwa wameketi katika maeneo yao saa tisa alasiri.
Hamad
alisema ratiba ya shughuli hiyo itaanza na kikao cha Bunge saa 9.10 na baadaye
kikao hicho kitaahirishwa saa 9.20 kwa ajili ya kumpokea Rais Kikwete.
Wageni mashuhuri
Hamad
alisema Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, amewaalika wageni mbalimbali
kushuhudia tukio hilo muhimu la kitaifa, wakiwemo viongozi wa kitaifa na watendaji
wakuu kutoka pande zote za Muungano.
Miongoni
mwa wageni mashuhuri watakaokuwepo ni pamoja na mjane wa Baba wa Taifa, Mama
Maria Nyerere na marais wastaafu Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar.
Wengine ambao wamealikwa kuhudhuria tukio hilo ni Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji mstaafu Joseph Warioba, wajumbe wenzake na makamishna wote wa Tume hiyo.
Pia watakuwepo viongozi wengine wastaafu wa kitaifa ambao ni mawaziri wakuu wastaafu, Waziri Kiongozi mstaafu na maspika wa Bunge.
Wageni
wengine walioalikwa ni kutoka taasisi za dini, taasisi zisizo za kiserikali,
wawakilishi wa tasnia ya habari, vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu na
taasisi za elimu ya juu.
Pia
vipo vyama vya watu wenye ulemavu, vyama vya wafanyakazi, vyama vya wafugaji,
vyama vya wavuvi na wakulima pamoja na wawakilishi kutoka sekta binafsi.
Kuwasili kwa JK
Baada
ya Rais kuwasili katika eneo la Bunge, atapokewa na Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti,
Katibu na Naibu Katibu wa Bunge Maalumu la Katiba na baadaye kwenda katika
jukwaa maalumu kupokea salamu za heshima na kukagua gwaride maalumu
lililoandaliwa na Polisi.
Katibu
wa Bunge alisema baada ya shughuli zote zitakazofanyika katika viwanja vya
Bunge kumalizika, utaratibu umewekwa kwa viongozi kuingia bungeni kwa
maandamano maalumu.
Viongozi
watakaotangulia ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Seif Sharif Hamad, Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dk Gharib Mohammed Bilal, Rais wa Zanzibar, Dk
Ali Mohammed Shein na Rais Kikwete ambaye atakuwa amefuatana na mwenyeji wake
ambaye ni Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samuel Sitta.
Baada
ya Rais kumaliza kuhutubia Bunge Maalumu, wajumbe wote wa Bunge Maalumu
watapata fursa ya kupiga picha ya pamoja mbele ya jengo la Bunge.
Rais
atalihutubia Bunge ili kutoa nafasi kwa bunge hilo kuendelea na mjadala baada
ya Jaji Warioba kuwasilisha rasimu ya pili ya Katiba, Jumanne wiki hii.
Hotuba
ya Jaji Warioba ambayo ilijaa tafiti nyingi inaonekana kuwachanganya wajumbe
wengi kwa kuamini kuwa imeibua mambo mengi ambayo yalikuwa yamefichika.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SERIKALI KUHAMIA DODOMA KESHO.”
Post a Comment