Thursday, March 20, 2014
MWANAFUNZI WA UDOM ALIYEJIRUSHA KUFIKISHWA MAHAKAMANI MARA BAADA YA TARATIBU KUKAMILIKA KWA KUJIBU TUHUMA ZA KUTAKA KUJARIBU KUJIUA.
Do you like this story?
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME |
Mwanafunzi wa Chuo Kikuu Dodoma – UDOM aitwae KAMUGISHA ISACK (24) Mhaya, Mwaka wa Tatu Kitivo cha Sayansi ya Jamii (Social Science) anayeishi Block Namba 11, chumba Namba 62, alijitupa kutoka ghorofa ya pili hadi chini na kusababisha majeraha sehemu za mdomoni, shingoni na kwenye paji la uso.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna msaidizi
mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME amesema hili tukio limetokea terehe
18/03/2014 saa mbili na robo chuo kikuu cha Dodoma
Amesema uchunguzi wa awali umeonyesha chanzo cha
tukio ni ulevi ambapo majeruhi alilazwa katika hospitali ya UDOM na baadaye
kuhamishiwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na kuruhusiwa tarehe 20/03/2014 baada
ya kuonekana hali yake inaendelea kuimarika.
Pamoja na hayo, Kamanda MISIME amesema mtuhumiwa
atafikishwa mahakamani baada ya kukamilisha taratibu zote kujibu shitaka
la kujaribu kujiua.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ MWANAFUNZI WA UDOM ALIYEJIRUSHA KUFIKISHWA MAHAKAMANI MARA BAADA YA TARATIBU KUKAMILIKA KWA KUJIBU TUHUMA ZA KUTAKA KUJARIBU KUJIUA.”
Post a Comment