Thursday, March 20, 2014

MWANAFUNZI WA UDOM ALIYEJIRUSHA KUFIKISHWA MAHAKAMANI MARA BAADA YA TARATIBU KUKAMILIKA KWA KUJIBU TUHUMA ZA KUTAKA KUJARIBU KUJIUA.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME




Mwanafunzi wa Chuo Kikuu Dodoma – UDOM aitwae KAMUGISHA ISACK (24) Mhaya, Mwaka wa Tatu Kitivo cha Sayansi ya Jamii (Social Science) anayeishi Block Namba 11, chumba Namba 62, alijitupa kutoka ghorofa ya pili hadi chini na kusababisha majeraha sehemu za mdomoni, shingoni na kwenye paji la uso.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME amesema hili tukio limetokea terehe 18/03/2014 saa mbili na robo chuo kikuu cha Dodoma 
Amesema uchunguzi wa awali umeonyesha chanzo cha tukio ni ulevi ambapo majeruhi alilazwa katika hospitali ya UDOM na baadaye kuhamishiwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na kuruhusiwa tarehe 20/03/2014 baada ya kuonekana hali yake inaendelea kuimarika.

Pamoja na hayo, Kamanda MISIME amesema mtuhumiwa atafikishwa mahakamani baada ya kukamilisha taratibu zote  kujibu shitaka la kujaribu kujiua.

0 Responses to “ MWANAFUNZI WA UDOM ALIYEJIRUSHA KUFIKISHWA MAHAKAMANI MARA BAADA YA TARATIBU KUKAMILIKA KWA KUJIBU TUHUMA ZA KUTAKA KUJARIBU KUJIUA.”

Post a Comment

More to Read