Tuesday, March 25, 2014
SERIKALI YAMTIMUA KAZI MKURUGENZI WA BODI YA UTALII NCHINI.
Do you like this story?
MKURUGENZI
Mtendaji wa Bodi ya Utalii (TTB), Dk Aloyce Nzuki amevuliwa madaraka kwa madai
ya utendaji usioridhisha pamoja na kusababisha Tanzania kuwa nyuma katika
masuala ya utalii.
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alitangaza uamuzi huo jana kwa
waandishi wa habari. Amesema hatua yake hiyo, imetokana na Bodi ya Utalii,
kumshauri amwondoe kazini mkurugenzi huyo.
Nyalandu
amesema alipokea barua iliyosainiwa na wajumbe wote wa Bodi ya Utalii,
wakimuomba amuondoe kazini Mkurugenzi huyo.
“Leo
(jana) baada ya kufanya kikao na wajumbe wa TTB, nimeridhia kuondolewa kazini
kwa Mkurugenzi huyo na Wizara itampangia kazi nyingine,” alisema Nyalandu.
Kikao
cha pamoja kati ya Bodi na Waziri Nyalandu, kilihudhuriwa pia na Naibu Waziri,
Mahamoud Mgimwa, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maimuna Tarishi
na Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Selestine Gesimba.
Kutokana
na uamuzi huo, kuanzia leo Bodi ya Utalii imeagizwa kutangaza nafasi ya kazi
hiyo na mwenye sifa atume maombi ndani ya siku 21.
Amesema
baada ya siku 21, TTB ichague kampuni zitakazohusika kuchambua watu wenye sifa.
Mchakato huo unaelekeza kampuni husika kupokea na hatimaye kupata majina tisa,
ambayo pia yatachambuliwa na kisha kuwasilisha wizarani majina matano.
Wizara
pia itachambua na kuwasilisha majina matatu kwenda kwa Rais, ambaye ndiye
mwenye mamlaka ya kuteua jina moja la Mkurugenzi wa bodi hiyo.
Wakati
huo huo Mkurugenzi wa Masoko, Devota Mdachi ameteuliwa kukaimu nafasi hiyo ya
ukurugenzi wa TTB hadi hapo mchakato wa kumpata mkurugenzi,
utakapomalizika.Nyalandu alisisitiza kwamba ni azma ya Serikali kuhakikisha
utalii unakwenda popote duniani.
Awali,
akizungumza, Mwenyekiti wa Bodi, Charles Sanga alisema Bodi hiyo ilimshauri
Waziri kumuondoa kazini Mkurugenzi huyo kutokana na kutokuwa na imani naye na
utendaji usioridhisha.
“Ili
Bodi ifanye kazi kwa ufanisi, inahitaji utendaji mzuri ambao utakuwa
umeboreshwa… hivyo tumemshauri Waziri, Dakta Nzuki aondoke, apishe nanafasi
yake ichukuliwe na mwingine, kwani hatuwezi kufanya naye kazi,” alisema Sanga.
CHANZOO:HABARI
LEO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SERIKALI YAMTIMUA KAZI MKURUGENZI WA BODI YA UTALII NCHINI.”
Post a Comment