Thursday, March 20, 2014
SITA YU MSALABANI, KUONGOZA BUNGE MAALUMU LA KATIBA.
Do you like this story?
Mkanganyiko pekee na uliobakia kwa
Watanzania wakiwamo wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba ni viporo kwenye
kanuni za 37 na 38, vinginevyo hali ya hewa ndani ya Bunge hilo imetulia.
Wajumbe wa Bunge hilo wapo tayari kuanza
kibarua cha kwanza cha kujadili Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya, kazi
ambayo hakuna shaka ndiyo iliyowaweka Dodoma.
Hata hivyo, kabla ya mwenyekiti mteule Samuel
Sitta kushinda kinyang’anyiro cha kuongoza Bunge hilo wiki iliyopita,
chama chake, CCM kimekuwa kikionekana kuwa na mkakati wa nguvu wa kushawishi na
hatimaye kupitisha mapendekezo na matakwa yake, yakiwamo ya Serikali mbili.
Sitta ambaye amechaguliwa kwa asilimia 86.5
ya kura za wajumbe ana mtihani mzito aliobebeshwa mabegani ukiwamo wa kutetea
msimamo wa chama chake au kuukana.
Akisaidiwa na Samia Suluhu Hassan ambaye naye
amechaguliwa kwa asilimia 74, wawili hawa wana kibarua mbele yao.
Yeye (Sitta), ni muumini wa Serikali mbili
kama ilivyo CCM, ingawa inaaminika kuwa amebadili msimamo kutoka ule wa awali
wa Serikali tatu.
Tayari, ameahidi mbele ya wajumbe kulinda
muungano kwa njia yoyote ile kupitia rasimu hiyo.
Mtego mpya kwake ndani ya Bunge ni imani
kubwa ambayo wajumbe hao wanayo kwake kwani bila kujali itikadi zao
wamempitisha kuwa mwenyekiti wao kwa idadi ya kura 487, sawa na asilimia 86.5
Hii ni ishara ya kumwamini kwamba,
atahakikisha anatetea masilahi ya Watanzania wote badala ya chama chake.
Matumaini hayo yanakuja baada ya kujijengea
uaminifu mkubwa kupitia uongozi wake wa Bunge la Tisa la Jamhuri ya Muungano
kupitia kaulimbiu yake ya ‘kasi na viwango’.
Wapo Watanzania wanaosema kuwa nafasi
hiyo kwa Sitta inaweza kumjengea umaarufu ama kumwondolea imani kwao, endapo
hatakuwa mwangalifu katika kuliongoza Bunge hilo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SITA YU MSALABANI, KUONGOZA BUNGE MAALUMU LA KATIBA.”
Post a Comment