Friday, March 21, 2014
WAKO: MSIPUUZE MAONI YA WANANCHI.
Do you like this story?
Mwanasheria Mkuu mstaafu wa Serikali ya Kenya, Seneta Amos Wako akizungumza jana, wakati wa Semina ya Bunge Maalumu la Katiba. Picha na Salim Shao |
Mwanasheria Mkuu (AG) mstaafu wa Kenya, Amos
Wako amewataka wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kutokupuuza maoni ya wananchi
katika kutunga Katiba ya nchi vinginevyo watazua mgogoro.
Wako, ambaye kwa sasa ni Seneta wa Busia ya
Mashariki nchini Kenya, alitoa ushauri huo jana katika semina kwa wajumbe wa
Bunge la Katiba kuhusu uzoefu wa namna nchi hiyo ilivyopitia misukosuko ya
kuipata Katiba mpya.
Wako ambaye kwa miaka 21 alikuwa katika
wadhifa wa AG, amesema matukio mengi yaliyosababisha Kenya kutokupata Katiba
yao kwa wakati, yalitokana na kutokuwashirikisha wananchi moja kwa moja katika
mchakato.
Katika hotuba yake iliyodumu kwa saa 2: 11,
mwanasheria huyo aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba ya Kenya alionya
pia kuwa Katiba inayotengenezwa hapa nchini isiwe ya kunukuu kutoka katika
mataifa mengine kwa sababu mahitaji yanatofautiana kwa kila nchi.
“Katiba isiwe ya mazungumzo kutoka kwa
viongozi pale Dar es Salaam, kwani itakuwa ni mali ya watu wachache na ambayo
lazima itapingwa, hata sisi tulianza hivyo lakini tulishindwa vibaya,” alionya
Wako.
Aliimwagia sifa Rasimu ya Katiba
iliyowasilishwa bungeni Jumanne iliyopita, kwamba kwa mtindo ilivyowasilishwa
inaonekana kuwajali na kuwapa nafasi zaidi wananchi wa hali ya chini.
“Pamoja na hayo, lakini Katiba hii
ikiingiliwa zaidi na kutekwa na wanasiasa au kikundi cha watu wachache kwa
masilahi yao, inaweza kuharibika kama ilivyotokea kwetu Kenya ambako Kanu
walikuwa wakipinga kila kitu wakatufanya tuingie katika mgogoro.”
Amesema kuwa mitazamo ya wanasiasa huwa ni
tatizo na hatari katika kutafuta Katiba mpya na dawa pekee na ya maana ni kutoa
nafasi kwa wananchi waamue wenyewe.
“Mfumo uliowekwa katika mchakato wa kuunda
Katiba mpya nchini kwenu, kwamba Rasimu ya mwisho ya Katiba itoke bungeni na
kupelekwa moja kwa moja kwa wananchi ni mzuri, ni muhimu maoni ya wananchi ya
awali yazingatiwe,” alisisitiza.
Kwa mujibu wa mwanasheria huyo, Bunge Maalumu
limeaminika kufanya kazi hiyo ili kuwasaidia wananchi kufikia malengo yao.
Akizungumzia uzoefu wa Kenya katika kupata
Katiba mpya alisema walianza kwa kukabiliana na changamoto kubwa ya ukabila
ambayo kila jamii ilikuwa haiamini kundi jingine katika kutafuta usawa, jambo
alilosema ni tofauti na Tanzania.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WAKO: MSIPUUZE MAONI YA WANANCHI.”
Post a Comment