Friday, March 21, 2014
WARIOBA AWAGONGANISHA KIFICHO NA MWAKILISHI.
Do you like this story?
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba. |
Hotuba ya Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya
Katiba, Jaji Joseph Warioba katika Bunge la Katiba imewagonganisha Spika
wa Baraza la Wawakilishi Pandu Ameir Kificho na Mwakilishi wa Baraza hilo,
Rufani Said Rufani.
Wakati Kificho akisisitiza kuwa Baraza hilo
halikupendekeza muundo wa serikali tatu, Warioba alieleza kwenye hotuba yake
kuwa kiini cha tume yake kupendekeza Muungano wa serikali tatu ni maoni ya
wananchi na taasisi mbalimbali, likiwamo Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
“Hii
inaonyesha kwamba Tume yenyewe ilishakuwa na mwelekeo wa serikali tatu kwa
sababu kama alivyoeleza Warioba kwamba walitafsiri maoni yetu kuwa ni yenye
kuhitaji serikali tatu na wakati mwingine, tafsiri inaweza kukupa maana tofauti
na maana halisi,” alieleza Kificho.
Kificho alisema Baraza hilo linaundwa na wawakilishi
kutoka vyama mbalimbali, CCM na CUF ambapo CCM msimamo wao ni serikali mbili na
kwamba hana uhakika kwa upande wa CUF, ingawa anadhani wana msimamo wa serikali
tatu.
Hata hivyo, Rufani, ambaye ni Mwakilishi wa
Jimbo la Tumbe kupitia CUF, alikubaliana na alichosema Jaji Warioba kuwa ndicho
kilichokubaliwa na baraza hilo.
“Ingawa sikuwa mjumbe katika kamati ya
uongozi kwa nafasi yangu ya uwakilishi naafikiana kuwa maoni yaliyosomwa na
Jaji Warioba bungeni ndiyo hasa tuliyopeleka na jinsi alivyoyatafsiri ndivyo
tulivyomaanisha,” alieleza Said.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WARIOBA AWAGONGANISHA KIFICHO NA MWAKILISHI.”
Post a Comment