Sunday, May 25, 2014
BAJETI KUU HATIHATI.
Do you like this story?
Wakati
Serikali ikiwa taabani kifedha, wabunge wengi, wakiwamo wajumbe wa Kamati ya
Bunge ya Bajeti wanapanga kukwamisha Bajeti Kuu ya Serikali, inayofikia zaidi
ya Sh19 trilioni.
Habari
kutoka ndani ya vikao vya Kamati ya Bunge ya Bajeti, zinadai kuwa iwapo
Serikali haitapunguza misamaha ya kodi hadi asilimia moja ya pato la taifa
(GDP), wabunge hao watakwamisha bajeti hiyo.
Mbunge
wa Mwibara, Kangi Lugola (CCM), alilithibitishia gazeti hili jana kuwa yeye ni
miongoni mwa wabunge waliopanga kukwamisha bajeti hiyo na yuko tayari kufukuzwa
ubunge kwa hilo.
Lugola
alisema kuwa pamoja na kuwepo kanuni inayowakataza wabunge wa CCM kukwamisha
bajeti na anayefanya hivyo hufukuzwa, yuko tayari afukuzwe ili ayaponye maisha
ya Watanzania milioni 45.
“Kila
mwaka tunapiga kelele misamaha ya kodi, wanatumia mwanya huo vibaya na matokeo
yake bajeti za Serikali mwaka hadi mwaka hazipati fedha kutoka Hazina,” alisema
Lugola na kuongeza:
Lugola
alisema kama Serikali haitakuja na mwarobaini wa misamaha ya kodi, ukwepaji wa
kodi, matumizi makubwa ya Serikali na kupambana na ufisadi na wizi, bungeni
hapatatosha.
Mbunge
wa Kasulu Mjini, Moses Machali (NCCR-Mageuzi), jana alisema kuwa angetamani
kama Bajeti ya Serikali isipite mwaka huu ili wabunge watimize wajibu wao wa
kikatiba wa kuisimamia Serikali.
“Nenda
kwenye Ripoti za CAG, madudu ni yaleyale mwaka hadi mwaka, misamaha ya kodi
ndiyo usiseme, matumizi ya anasa ndiyo balaa. Nchi inakwenda wapi?” alihoji
Machali na kuongeza:
“Kama
kweli wabunge wanaitakia mema nchi hii, tuungane, kama Serikali haiji na majibu
ya madudu yote haya tusipitishe bajeti hii. Tuweke historia ambayo vizazi
vijavyo vitatukumbuka.”
Wakati
wabunge wengi wakipanga kukwamisha bajeti iwapo misamaha hiyo haitapunguzwa
hadi asilimia 1 ya GDP, hadi kufikia Juni 30, 2013 misamaha hiyo ilikuwa Sh1.52
trilioni.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “BAJETI KUU HATIHATI.”
Post a Comment