Wednesday, June 4, 2014
CAR YABANA UJUMBE MFUPI (SMS)
Do you like this story?
Maafisa
wa utawala Katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, wamebana matumizi ya ujumbe mfupi
wa simu za mkononi baada ya kusema kuwa ni tisho kwa usalama wa nchi.
Taarifa
hii ni kwa mujibu wa waziri wa mawasiliano serikali.
Watumiaji
wa simu za mkononi ambao wamekuwa wakijaribu kutuma ujumbe mfupi wanapata jibu
hili: ''Ujumbe wako hauwezi kutumwa.''
''Wenye
simu za mkononi hawaruhusiwi kutuma ujumbe mfupi kuanzia Jumatatu 2 Juni hadi
itakapotolewa taarifa zaidi kuhusu agizo hili,'' huu ndio ulikuwa ujumbe wa
wizara ya mawasiliano kwa kampuni za kutoa huduma za simu.
Inaarifiwa
kuwa uamuzi huo ulifikiwa na waziri mkuu Andre Nzapayeke.
Tangu
wiki iliyopita, kumekuwa na ghasia zaidi mjini Bangui, pamoja na kutolewa wito
wa maandamano uliotumwa kwa simu kama ujumbe mfupi siku chache zilizopita.
Duru
zinasema kuwa hatua ya kubana ujumbe mfupi wa simu itadumu kwa siku kadhaa
kabla ya agizo lengine kubatilisha amri hiyo.
Jamhuri
ya Afrika ya Kati ambayo inakumbwa na vita kati ya jamii za wakristo na
waisilamu imekuwa ikikumbwa na hali ngumu ya usalama pamoja na mashambulizi ya
kulipiza kisasi kati ya jamii hizo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “CAR YABANA UJUMBE MFUPI (SMS)”
Post a Comment