Wednesday, June 4, 2014
VITENDO VYA UKEKETAJI NA MIGOGORO YA NDOA VYAPUNGUA WILAYANI MAKETE.
Do you like this story?
Imeelezwa kuwa Matatizo ya ukeketaji na
migogoro ya ndoa yamepungua wilayani Makete kutokana elimu iliyotolewa kwa
wananchi na shirika lisilo la kiserikali la MASUPHA wakishirikiana na The
Foundation for Civil Societies katika kata tano za wilaya hiyo
Akizungumizia kuhusu hilo mkurugenzi wa
MASUPHA Bi Aida Chengula amesema mradi huo uliokuwa unadhaminiwa na shirika
la The Foundation For Civil Societies ambao umetekelezwa katika
kata tano ambazo ni Ukwama, Mang’oto,Kipagalo,Ikuwo,na Mfumbi zote za
wilayani Makete
Pia amesema mradi huo ulianza Decemba
27 mwaka 2013 “mradi wetu tumeutekeleza katikakata tano ambapo kila kata
tulimujengea uwezo kijana mmoja kwaajili ya kutoa elimu kwa jamii inayo
mzunguka kuhusiana na mambo sera ya taifa ya Ukimwi,unyanyasaji wa kijinsia,na
elimu kuhusu unyanyasaji wa kijinsia hususan ukeketaji kwa wanawake”
Bi Chengula alielezea faida walizo
zipata katika mradi huo kuwa malengo yao yametimia kwani idadi kubwa ya
mambo waliyolenga yametekelezeka ikiwemo kupunguza idadi ya kesi za migogoro ya
kifamilia katika mabaraza ya usuluhishi katika kata tano ambazo mradi ulikuwa
unatekelezwa na kuongeza kuwa jamii ilikuwa haina elimu kuhusina na mambo ya
ndoa ambayo mpaka kiasi Fulani imepungua kutoka kesi 5 hadi 8 kwa mwezi
na kufikia kesi 1 hadi 2 kwa mwezi
Hata hivyo Bi Chengula ameiambia blog
hii kuwa licha ya mradi huo kuwa na mafanikio amezitaja changamoto za mradi huo
kuwa ni pamoja na watu kuwa na uelewa mdogo wakati wa warsha mbalimbali
kwani wamekuwa wakitaka kulipwa fedha nyingi
“Makete kuna mashirika mengi yanayotoa
elimu hivyo watu wamekuwa wakilinganisha viwango vya posho kutoka katika
mashirika mengine hivyo kufanya mwitikio wa jamii kuwa
mdogo”alisema Bi Chengula na kuongeza kuwa pia kumekuwa na changamoto
ya pesa za mradi kutokufika kwa wakati.
Kwa upande wao vijana waliokuwa wakitoa
elimu katika vijiji vya kata zao walieleza kufurahishwa na mradi huo kwani licha
ya kusaidia elimu kwa jamii pia wao wamejengewa uwezo ambao
utawasaidia kujijengea familia bora
“mradi huu umewasaidia wanajamii
kubadilika kwa kiasi kikubwa hapa katika kata yetu kumekuwa na tatizo la
akina mama wenye umri mkubwa kujihusisha na mapenzi na vijana wadogo jambo
ambalo limekemewa na elimu imetolewa na kumekuwa na mabadiliko kwa jamii
hiyo”alisema Neema Sanga muwezeshaji kutoka katika kata ya Ukwama
Naye Frojensia Sage mwezashaji
kutoka katika kata ya Nkondo alisema kama kijana ametoa elimu katika kata
hiyo na kumesadia kubadilika husasani suala ukeketaji kwa wanawake ambapo
mpaka sasa jamii hiyo imeweza kubadilika pia aliongeza kuwa kumekuwa na
changamoto za za utekelezaji ikiwemo vitendea kazi kama vipeperushi
ambavyo vinaweza kusaidia jamii pia kujijengea utaratibu wa kupata elimu
kupitia maandishi kwani yanahifadhika kwa muda mrefu
Bw. Sage alisema pia viongozi wa maeneo
husika wamekuwa hawatoi ushirikiano kwa wawezeshaji hao hao
Na
Riziki Manfred
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “VITENDO VYA UKEKETAJI NA MIGOGORO YA NDOA VYAPUNGUA WILAYANI MAKETE.”
Post a Comment