Wednesday, June 4, 2014
POLISI NA MASHEIKH WAVUTANA KUHUSU PICHA YA MAREHEMU NASRA KUWEKWA KWENYE JENEZA
Do you like this story?
Mvutano mkali umezuka kwenye shughuri
ya kuaga mwili wa Marehemu Nasra Mvungi kati ya Polisi,maafisi Ustawi na
Masheikh kuhusu picha ya marehemu Nasra kuwekwa kwenye Jeneza wakati
wa kuaga mwili wake kwenye Uwanja wa Jamhuri Jana.
Maafasi wa kike wa
Polisi wa Dawati la Jinsia na maafisi wa Ustawi wa Jamii mkoa walikuza Picha ya
Marehemu Nasra kwa lengo la kuiweka kwenye Jeneza jambo lililopingwa vikali na
viongozi wa dini ya Kiislam wakida jambo hilo ni kinyume na sheria za dini yao.
Hata hivyo baada ya
mvuta huo uliodumu kwa dakika 15 ulifikia muafaka baada ya Polisi na maafisi
Ustawi kupokea busara za mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini Bw Fikiri
Juma aliyeingilia kati mvutano huo walikubali kutoiweka Picha hiyo ya marehmu
kwenye Jeneza,
Mmoja wa mapolisi hao
aliamu kuichukua kwa uchungu picha hiyo na kuiweka kwenye mkoba wake huku
akiseme” Kama wamekataa basi tutaenda kuiweka kwenye Ofisi zetu kama kumbukumbu
ya mtoto wetu Nasra”alisema kwa Uchungu Afande huyo.
Akizungumza kwenye
hafra hiyo Kaimu Sheikh mkuu wa Mkoa wa Morogoro Sheikh Ally Omar alisema
Ingawa tukio hilo la kumuaga Nasra limefanyika Kiserikali haimaanishi kuvunja
sheria za dini kwa kuweka picha ya marehemu kwenye Jeneza
“ Mbali ha kuzia
Picha hiyo kuwekwa Kwenye Jeneza laki pia Kisheria sisi hatuna mambo ya kuga
tukivunja sheria za dini nini nitaulizwa na wakubwa zangu,hivyo kwa sasa sote
tusimane na tutaga mwili wa Nasra kwa kusoma dua na baada ya hapo tutaelekea
msikiti kuuswalia mwili wa marehemu na baadae kwenda kuuzika.
Marehemu Nasra ambaye
alifichwa kwenye Boksi kwa zaidi ya miaka 3 na mama yake Mkubwa Bi Mariam Said
alifichuliwa na wasamalia wema May 25 mwaka huu na kutibiwa katika hospital ya
mkoa wa Morogoro kabla ya kuhamishi hospital ya Tifa Muhimbili ambako Jumapili
iliyopita alifariki dunia na kuzikwa jana makabuli ya mkoa mkoani hapa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “POLISI NA MASHEIKH WAVUTANA KUHUSU PICHA YA MAREHEMU NASRA KUWEKWA KWENYE JENEZA ”
Post a Comment