Wednesday, June 4, 2014
ASHA BARAKA ADAI HAWEZI KUMSAMEHE ALLY CHOKI
Do you like this story?
MKURUGENZI wa Bendi ya African
Stars ‘Twanga Pepeta’ Asha Baraka, amesema kamwe hawezi kumsamehe mwanamuziki
Ally Choki ambaye ni Mkurugenzi wa Bendi ya Extra Bongo, ambaye ana bifu naye
la muda mrefu.
Hivi
karibuni habari zilienea kuwa wawili hao wameshapatana baada ya kukutanishwa na
chombo kimoja cha habari nchini, jambo ambalo Asha amelikanusha.
“Siwezi
kupatana na Choki kwa sababu sioni haja ya kufanya hivyo. Nimesikia kwenye
mitandao kuwa eti tumepatanishwa... watu bwana! Labda waliopatana ni wao siyo
mimi. Nasisitiza habari hizo ni za uongo na ninaomba Choki akae mbali na mimi,”
alisema Asha.
Kwa
upande wa Choki, alipoelezwa kuhusiana na majibu ya Asha, alicheka kisha
akasema: “Kama yeye amesema hivyo, acha iwe hivyohivyo. Kwanza hayo mapatano
yenyewe sijafanya kwa ajili yake maana hakuna kitu ninachotaka kwake. Nina
mambo mengi ya kufanya.”
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ASHA BARAKA ADAI HAWEZI KUMSAMEHE ALLY CHOKI ”
Post a Comment