Wednesday, June 4, 2014
MAJANGA: WANAWAKE RUKWA WATUMIA KONDOMU KAMA BANGILI.;
Do you like this story?
BAADHI ya wanawake mkoani Rukwa
wamebadili matumizi ya kondomu za kike kwa kuzivaa kama urembo wa bangili.
Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya kiserikali
ya Rodi inayohusika na kutoa elimu kwa jamii ya njia sahihi ya kutumia kondomu
ili kujikinga na maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU), Gideon Mpina aliyasema
hayo jana,
\
Alikiri kuwa matumizi sahihi ya kondomu
za kike ni changamoto kubwa mkoani humo, kwa kuwa kondomu hizo zina umbo la
bangili na baadhi ya wanawake wanazitumia kuvaa mikononi kama urembo.
“Bangili za kondomu hizo zimekuwa
kivutio kikubwa kwa wanawake. Wanazivaa mikononi kama urembo kwani zinapendeza
machoni sababu zikipigwa na mionzi ya jua zinabadili rangi mbalimbali na kuwa
kivutio cha aina yake,” alisema Mpina.
Alisema imekuwa changamoto kubwa kwa
Rodi kwani licha ya kuisambaza bila malipo bado baadhi ya wanawake wanazitumia
na wengine kuzinunua kutoka kwa wenzao ili tu wapate bangili.
Rodi pia inatoa elimu kuhusu malaria
mkoani hapa kwa kushirikiana na halmashauri za wilaya na manispaa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MAJANGA: WANAWAKE RUKWA WATUMIA KONDOMU KAMA BANGILI.;”
Post a Comment