Wednesday, June 4, 2014
MAWAZIRI SABA MAHUTUTI.
Do you like this story?
Msuguano
mkali umekuwa wakati Bunge linapokaa kama kamati kupitia vifungu vya bajeti za
wizara husika. Hata hivyo, bajeti hizo zimepitishwa baada ya maelezo marefu na
wakati mwingine msaada wa kiti cha Spika au pale Waziri Mkuu au Kaimu wake
ndani ya Bunge anaposimama ‘kuokoa jahazi’.
\
Mawaziri
ambao hadi sasa wameingia katika orodha ya bajeti zao kupita kwa mbinde na
wizara zao kwenye mabano ni Profesa Jumanne Maghembe (Maji), Profesa Anna
Tibaijuka (Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi), Profesa Sospeter Muhongo
(Nishati na Madini), Dk John Magufuli (Ujenzi), Dk Harrison Mwakyembe
(Uchukuzi), Sophia Simba (Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto) na Dk Seif
Rashid
(Afya
na Ustawi wa Jamii).
Kwa
sehemu kubwa, bajeti nyingi zilipata upinzani kutokana na Hazina kutoa fedha
kidogo za maendeleo kati ya asilimia 19 na 30 tu, wakati wizara nyingine
zilitikiswa na tuhuma za ufisadi wa watendaji wake.
Miongoni
mwa mivutano ni ule uliohusu taasisi ya Wanawake na Maendeleo (Wama) ambayo
Mwenyekiti wake ni mke wa Rais Jakaya Kikwete, Mama Salma, hoja iliyoibuka
wakati wa mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.
Mbunge
wa Ole (CUF), Rajab Mbarouk Mohamed alitaka taasisi hiyo ifutwe, kwa maelezo
kwamba inajihusisha na masuala ya kisiasa na kwamba mwaka 2010, Mama Salma
aliitumia kumfanyia kampeni mumewe.
Katika
hoja hiyo alisema mmoja wa wajumbe wa bodi ya taasisi hiyo ni Waziri wa wizara
hiyo, Sophia Simba kinyume na sheria na taratibu.
Waziri
Simba akajibu: “Nipo Wama lakini kazi ninayoifanya pale ni ya kujitolea na
silipwi kitu. Kanuni na sheria zinakataza mtu kujihusisha na taasisi nyingine
kama tu anakuwa analipwa mshahara”.
Juzi,
Profesa Maghembe alipata wakati mgumu baada ya hoja iliyoshika mshahara wake
iliyotolewa na Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika kujadiliwa kwa dakika
31, hadi Kaimu Waziri Mkuu, Profesa Mark Mwandosya alipoingilia kati.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MAWAZIRI SABA MAHUTUTI.”
Post a Comment