Wednesday, June 4, 2014

MAWAZIRI SABA MAHUTUTI.



Msuguano mkali umekuwa wakati Bunge linapokaa kama kamati kupitia vifungu vya bajeti za wizara husika. Hata hivyo, bajeti hizo zimepitishwa baada ya maelezo marefu na wakati mwingine msaada wa kiti cha Spika au pale Waziri Mkuu au Kaimu wake ndani ya Bunge anaposimama ‘kuokoa jahazi’.
\
Mawaziri ambao hadi sasa wameingia katika orodha ya bajeti zao kupita kwa mbinde na wizara zao kwenye mabano ni Profesa Jumanne Maghembe (Maji), Profesa Anna Tibaijuka (Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi), Profesa Sospeter Muhongo (Nishati na Madini), Dk John Magufuli (Ujenzi), Dk Harrison Mwakyembe (Uchukuzi), Sophia Simba (Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto) na Dk Seif Rashid
(Afya na Ustawi wa Jamii).

Kwa sehemu kubwa, bajeti nyingi zilipata upinzani kutokana na Hazina kutoa fedha kidogo za maendeleo kati ya asilimia 19 na 30 tu, wakati wizara nyingine zilitikiswa na tuhuma za ufisadi wa watendaji wake.

Miongoni mwa mivutano ni ule uliohusu taasisi ya Wanawake na Maendeleo (Wama) ambayo Mwenyekiti wake ni mke wa Rais Jakaya Kikwete, Mama Salma, hoja iliyoibuka wakati wa mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.
Mbunge wa Ole (CUF), Rajab Mbarouk Mohamed alitaka taasisi hiyo ifutwe, kwa maelezo kwamba inajihusisha na masuala ya kisiasa na kwamba mwaka 2010, Mama Salma aliitumia kumfanyia kampeni mumewe.

Katika hoja hiyo alisema mmoja wa wajumbe wa bodi ya taasisi hiyo ni Waziri wa wizara hiyo, Sophia Simba kinyume na sheria na taratibu.
Waziri Simba akajibu: “Nipo Wama lakini kazi ninayoifanya pale ni ya kujitolea na silipwi kitu. Kanuni na sheria zinakataza mtu kujihusisha na taasisi nyingine kama tu anakuwa analipwa mshahara”.

Juzi, Profesa Maghembe alipata wakati mgumu baada ya hoja iliyoshika mshahara wake iliyotolewa na Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika kujadiliwa kwa dakika 31, hadi Kaimu Waziri Mkuu, Profesa Mark Mwandosya alipoingilia kati.

0 Responses to “MAWAZIRI SABA MAHUTUTI.”

Post a Comment

More to Read