Wednesday, January 21, 2015
SHUGULI ZA BIASHARA ARUSHA ZASIMAMA KWA SABABU YA MGOMO.
Do you like this story?
Shuguli mbalimbali ndani ya jiji
la Arusha zikiwemo za kibiashara jana(leo)zimelazimika kusimama mara baada ya
mabasi ya abiria (Daladala) kugoma kubeba abiria kwa madai kuwa utaratibu wa
Ruti ndefu zilizopangwa na Sumatra ni uonevu mkubwa
hataivyo kugoma kwa daladala hizo
pia kuliweza kuwaaathiri wanafunzi ambao wanatumia usafiri huo kwa ajili ya
kwenda mashuleni hali ambayo iliwafanya wakose masomo lakini pia baadhi yao
wafike mashuleni wakiwa wamechelewa.
Akiongea kwa niaba ya madereva
daladala ambao wamegoma dereva,Jumaa isa alisema kuwa wanashangazwa sana na
Sumatra kuweza kuwapangia Ruti ndefu wakati bado hata abiria wa Jiji la Arusha
hawana uwezo wa kutumia hizo ruti ndefu.
Jumaa alisema kuwa kwa historia
ya mji wa Arusha abiria wanakuwepo majira ya asubui na jioni kwa pekee ila kwa
majira ya mchana abiria ni wachache sana sasa hali hiyo inafanya mparangano mkubwa
sana barabarani.
aliendelea kwa kusema kuwa hapo
awali kulikuwa na vikao ambavyo vilifanyika lakini hakuweza kukubalina muafaka
wa ruti ndefu ambazo Sumatra walikuwa wanazitaka kitu cha kushangaza ni kwamba
tayari wameshaambiwa kuanza ruti ndefu jambo ambalo wamelipinga.
katika hatua nyingine akiongea
kwa niaba ya abiria Bi Neema Palangyo kutoka katika eneo la kwa Muorombo
alisema kuwa mgomo huo umesababisha madhara makubwa sana kwa wananchi wa Arusha
kwani uzalishaji wa siku hiyo ya mgomo ni mkubwa sana.
Hataivyo zaidi ya daladala mia
tano ambazo zote zinafanya shuguli zake za usafiri jijini Arusha ziliweza
kugoma na kisha kupinga azimio hilo la ruti ndefu ambalo lilitolewa kwa
kushirikiana na wadau wote wa Sumatra na usafirishaji Jijini Arusha.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SHUGULI ZA BIASHARA ARUSHA ZASIMAMA KWA SABABU YA MGOMO.”
Post a Comment