Wednesday, January 21, 2015
WANAHABARI NCHINI KUALIKWA KUJIFUNZA ATHARI ZA VITA SUDANI KUSINI.
Do you like this story?
Na Gladness Mushi-Ngurudoto Arusha
Waandishi wa habari kutoka katika
vyombo mbalimbali nchini Tanzania wanatarajiwa kuipelekwa nchini Sudan
Kusini ili kujifunza athari za vita ambazo zimetokea katika nchi ya
Sudani kusini.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu
mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana,leo wakati
akizungumza na waaandishi wa habari katika hafla ya utiaji saini baina
ya vikundi vinavyogombana kutoka nchini Sudani.
Kinana amesema kuwa baada ya
kuwekeana saini na makubaliano ya kuacha mapigano basi Nchi ya Tanzania
itachukua jukumu la kupekeka waaandishi wa habari Sudani kwa malengo ya
kujifunza na kujionea athari za vita .
“Tunataka waandishi wetu wa habari kutoka Tanzania wapate uelewa wa kutosha katika kuandika na kutangaza madhara
vita vya wenyewe kwa wenyewe, Kinana aliahidi kuwa ni muhimu na atahakikisha
anawapeleka waandishi wa habari waitembelee Sudan Kusini,”alisema.
Kinana alifafanua kuwa yeye binafsi anaamini watakapokwenda kujionea kwa macho madhara ya vita
wataweza kutumia vema kalamu zao kuelimisha watanzani
Chama Cha Mapinduzi (CCM)
kiliombwa kufanya na kusimamia mazungumzo juu ya vita hiyo na ndivyo watakavyofanya
pia kwa waandishi ili wapate somo.
Alisema mapigano hayo yamesababisha uchumi wa nchi hiyo kurudi nyuma
ukizingatia kuwa wao ni wazalishaji wakubwa wa ng’ombea na watatu
katika nchi za Afrika kwa kuwa na idadi kubwa ya mifugo ambapo pia wana utajiri mkubwa wa mafuta.
alisema Sudan Kusini ilihangaika miaka zaidi ya 50 kutafuta uhuru wao, miaka
miwili baada ya kujitenga kutoka Sudan Kaskazini, baada ya asilimia
90% kupiga kura ya kujitenga wakaanza vita ya kugombea madaraka, sasa
kila familia imeathirika kutokana vita ndio wanasaka amani.
Mazungumzo ya kutafuta amani kwa nchi hiyo yalianza mapema Desemba 23
na 24 mwaka jana 2014 katika Hotel ya Ngurudoto, Wilayani Arumeru,
Mkoan Arusha, huku zikiwakutanisha pande zote tatu zinazopigana kwa
ajili ya kusaka madaraka
Katika mazungumzo hayo mwenyekiti wa mazungumzo hayo ni Balozi Dk.
John Samwel Malecela, ambaye pia alikuwa ni Waziri Mkuu Mstaafu awamu
ya pili ya uongozi wa Rais Ally Hassan Mwinyi
Mapigano hayo ya ndani ya chama cha SPLM katika nchi ya Sudani Kusini
yanahusisha makundi matatu ambapo kila kundi linataka madaraka ya
kuongoza nchi hiyo.
Waandishi wa habari kutoka katika
vyombo mbalimbali nchini Tanzania wanatarajiwa kuipelekwa nchini Sudan
Kusini ili kujifunza athari za vita ambazo zimetokea katika nchi ya
Sudani kusini.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu
mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana,leo wakati
akizungumza na waaandishi wa habari katika hafla ya utiaji saini baina
ya vikundi vinavyogombana kutoka nchini Sudani.
Kinana amesema kuwa baada ya
kuwekeana saini na makubaliano ya kuacha mapigano basi Nchi ya Tanzania
itachukua jukumu la kupekeka waaandishi wa habari Sudani kwa malengo ya
kujifunza na kujionea athari za vita .
“Tunataka waandishi wetu wa habari kutoka Tanzania wapate uelewa wa kutosha katika kuandika na kutangaza madhara
vita vya wenyewe kwa wenyewe, Kinana aliahidi kuwa ni muhimu na atahakikisha
anawapeleka waandishi wa habari waitembelee Sudan Kusini,”alisema.
Kinana alifafanua kuwa yeye binafsi anaamini watakapokwenda kujionea kwa macho madhara ya vita
wataweza kutumia vema kalamu zao kuelimisha watanzani
Chama Cha Mapinduzi (CCM)
kiliombwa kufanya na kusimamia mazungumzo juu ya vita hiyo na ndivyo watakavyofanya
pia kwa waandishi ili wapate somo.
Alisema mapigano hayo yamesababisha uchumi wa nchi hiyo kurudi nyuma
ukizingatia kuwa wao ni wazalishaji wakubwa wa ng’ombea na watatu
katika nchi za Afrika kwa kuwa na idadi kubwa ya mifugo ambapo pia wana utajiri mkubwa wa mafuta.
alisema Sudan Kusini ilihangaika miaka zaidi ya 50 kutafuta uhuru wao, miaka
miwili baada ya kujitenga kutoka Sudan Kaskazini, baada ya asilimia
90% kupiga kura ya kujitenga wakaanza vita ya kugombea madaraka, sasa
kila familia imeathirika kutokana vita ndio wanasaka amani.
Mazungumzo ya kutafuta amani kwa nchi hiyo yalianza mapema Desemba 23
na 24 mwaka jana 2014 katika Hotel ya Ngurudoto, Wilayani Arumeru,
Mkoan Arusha, huku zikiwakutanisha pande zote tatu zinazopigana kwa
ajili ya kusaka madaraka
Katika mazungumzo hayo mwenyekiti wa mazungumzo hayo ni Balozi Dk.
John Samwel Malecela, ambaye pia alikuwa ni Waziri Mkuu Mstaafu awamu
ya pili ya uongozi wa Rais Ally Hassan Mwinyi
Mapigano hayo ya ndani ya chama cha SPLM katika nchi ya Sudani Kusini
yanahusisha makundi matatu ambapo kila kundi linataka madaraka ya
kuongoza nchi hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WANAHABARI NCHINI KUALIKWA KUJIFUNZA ATHARI ZA VITA SUDANI KUSINI.”
Post a Comment