Tuesday, January 20, 2015

WAFANYABIASHARA MBEYA WAZUA TAFRANI, WAANDAMANA MAHAKAMANI.




Wafanyabiashara zaidi ya 1000 wanaondesha shughuli zao za kibiashara katika masoko matano yaliyopo Jijini Mbeya, wakiwa nje ya mahakama ya Mwanzo ya Mbeya mjini, wakishinikiza mahakama hiyo kumuachia huru, Mwenyekiti wa Soko la Soweto  Honola Mbogella ambaye alifikishwa mahakamani hapo na halmashauri ya jiji la Mbeya kwa tuhuma za kuzuia watumishi wa umma kufanya kazi zao






Mmoja wa viongozi wa wafanyabiashara hao Ndugu Charles Syonga akizungumza na wafanyabiashara hao mara baada ya kumaliza mazungumzo na uongozi wa mkoa juu ya kumaliza tatizo



Jeshi la Polisi likiimalisha ulinzi katika eneo hilo(Picha na Fahari news)



(Fahari news)

MWENYEKITI wa Soko la Soweto jijini Mbeya,  Honola 
 Mbogella, amefikishwakatika  mahakama ya Mwanzo Mbeya mjinikwa tuhuma za kuzuia watumishi wa umma kufanya kazi zao. Kufuatia kukamatwa kwaMwenyekiti huyo kulisababisha zaidi  yawafanyabiashara 1000 wanaondesha shughuli zao za kibiashara katika masokomatano yaliyopo Jijini Mbeya, 

kuandamana na kuizunguka mahakama ya Mwanzo yaMbeya mjini, wakishinikiza mahakama hiyo kumuachia huru. Mwenyekiti huyo,amefikishwa  katika mahakama ya Mwanzo yaMbeya mjini, leo na kesi yake kusikilizwa majira ya saa tatu asubuhi  ambapo kesi hiyo ilivuta hisia za watukutokana na kundi hilo la wafanyabiashara kuizunguka mahakama hiyo, huku jeshila polisi likilazimika kuimarisha ulinzi. Akisomea mashitaka hayo Mbele  ya Hakimu wa Mahakama ya mwanzo ya Mbeya MjiniUbaswege Mathew, karani wa Mahakama hiyo, Sioni Kasunga, alisema mtuhumiwa huyoalifanya kosa hilo January 10 mwaka huu akiwa katika eneo

lake la kazi la Sokola Soweto lililopo Jijini Mbeya. Alisema, kwa mujibu wa kifungu kidogocha  cha sheria namba 101(a) sura ya 288iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002, mtuhumiwa aliwazuia watumishi wa umma wahalmashauri ya Jiji la Mbeya kufanya kazi yao ya kukusanya ushuru.

 Alisema, mtuhumiwa aliwazuiawafanyabiashara hao  kugoma kutozwaushuru wa shilingi 200 hadi 300 na halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa maelezokwamba  licha ya wafanyabiashara hao kulipiatozo hiyo kwa kipindi kirefu bado soko hilo limeendelea kukithiri kwa uchafu. Aidha, kutokana na kosa hilo,Hakimu wa mahakama hiyo, Ubaswege Mathew,baada ya kusikiliza maelezo hayo,alitoanafasi kwa mtuhumiwa ambaye alikana shitaka hilo hivyo, hakimu kuhairisha kesihiyo mpaka kesho(leo) na kwamba dhamana kwa  mtuhumiwa ipo wazi.


amesema Wakati kesi hiyo ikiendeleamahakamani hapo, umati mkubwa wa wafanyabiashara wanaoendesha shughuli zaokatika masoko matano ya Soweto,Uyole, Mabatini, Sokomatola na Uhindini ulijitokeza na kuizunguka mahakama hiyo kwa kile walichokidai kwamba   Mwenyekityi huyo ameonewa. Wakizungumza na Fahari news ,nje ya mahakama, wafanyabiashara hao ambao waligoma kutaja majina yao, walisema wao wamegoma kulipa ushuru huo kutokana na halmashauri kushindwa kuetekeleza majukumu yao ya ukarabati wa miundombinu pamoja na usafi wa mazingira hivyo Mwenyekiti huyo hausiki na  suala lakuwashawishi kugoma kama inavyodaiwa na halmashauri.  Hata hivyo, wafanyabiashara haowamegoma kuendelea na shughuli zao mpaka suala hilo litakapo patiwa ufumbuzikwa halmashauri kurekebisha miundombinu na usafi wa mazingira katika maeneo yabiashara.
 Mwisho.

0 Responses to “ WAFANYABIASHARA MBEYA WAZUA TAFRANI, WAANDAMANA MAHAKAMANI.”

Post a Comment

More to Read