Thursday, January 29, 2015
WAFANYABIASHARA JIJI LA MBEYA WAFUNGA MADUKA KWA KUPINGA KODI.
Do you like this story?
Maduka yakiwa yamefungwa |
Wafanyabiasha katika jiji la Mbeya wakiwa katika Mkutano wa kujadili kupanda kwa Kodi. |
Kaimu Meneja wa Tra Mkoa Bw Anniny Lema akijibu kero za wafanyabiashara kuhusiana na kupanda kwa kodi. |
Mmoja wa wafanyabiashara akitoa kero zake mbele ya Viongozi wa Tra katika Ukumbi wa Mkapa Jijini Mbeya. |
(Picha na Fahari News)
Wakazi wa jiji la Mbeya wamekumbwa na adha ya
kukosa huduma kwa ajili ya mahitaji mbalimbali baada ya
wafanyabiashara kufunga masoko na maduka yao yote, kwa ajili ya
kushiriki mkutano waliouitisha kwa ajili ya kujadili kodi ya TRA
inayodaiwa kuongezeka kwa asilimia 100.
Wafanyabiashara wa masoko na Maduka jiji la Mbeya jana
walikubalina kusitisha kufanya biashara kwa siku nzima kwa ajili ya kushiriki
katika mkutano huo ulioshirikisha zaidi ya wafanyabishara 1000 uliofanyika
katika ukumbi wa Benjamin Mkapa jijini hapa.
Wakuzingumza kwa nyakati tofauti baadhi ya
wakazi wa jiji la Mbeya walisema kuwa hali ni mbaya kutokana na kukosa
huduma kwa ajili ya mahitaji ya kila siku hasa bidhaa za vyakula.
“Kwa leo hali ni mbaya hakuna biashara yoyote
chakula inayofanyika maduka na masoko yamefungwa,mara baada ya
kuuliza wanatueleza kuwa wafanyabiashara wako kwenye mkutano hivyo
familia zetu zimeathirika kwani baadhi yetu hatuwezi kupata chakula kwa
siku ya leo”alisema
Naye Joel Mwakyoma mfanyabiashara kutoka Makongorosi
Wilayani Chunya alisema kuwa amesikitrishwa na hali aliyoikuta katika soko la
sido kwani ndiyo soko analolitegemea kwa ajili ya kununua bidhaa za jumla kwa
ajilli ya kwenda kuuza Chunya.
“Nimefika mapema leo saa 2:00 kutoka Chunya kwa
ajili ya kuja hapa soko la sido kwa ajili ya kujumua mahitaji ya duka langu
lakini nimekuta soko na maduka yote yamefungwa hivyo natakiwa kurudi chunya au
kulala hapa hadi kesho kitu ambacho ni hasara kwa biashara yangu”alisema
Mwakyoma ameishauri Serikali kupitia mamlaka ya mapato
Tanzania (TRA)kumaliza mgogoro baina yake na wafanyabiashara ili kuweza kuondoa
adha na migongano isiyo ya lazima ili kunusuru uvunjifu wa amani ambao unaweza
kutokea hapo baadae.
Mwisho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WAFANYABIASHARA JIJI LA MBEYA WAFUNGA MADUKA KWA KUPINGA KODI.”
Post a Comment