Friday, February 6, 2015
PINDA AZUA TENA!
Do you like this story?
Kauli ya
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuwa wanafunzi walioshiriki gwaride na halaiki
kwenye sherehe za miaka 38 ya CCM mjini Songea ni watoto wa wanachama wa chama
hicho, imekosolewa na wananchi na wabunge ambao walifikia uamuzi wa kuomba
mwongozo.
Sherehe hizo
zilifanyika Jumapili ya Februari Mosi kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea,
zikishirikisha makundi mbalimbali, wakiwamo wanafunzi wa shule za msingi na
sekondari ambao walivalia sare za CCM na kuimba nyimbo za chama hicho huku
wakicheza gwaride na halaiki, ambayo kwa kawaida huchukua muda mrefu kujifunza
na kuielewa.
Akijibu swali
la Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Susan Lyimo, mtendaji huyo mkuu wa
Serikali alitetea ushiriki wa watoto hao wapatao 500 kwenye sherehe hizo
akisema ni sehemu ya mfumo wa wanachama wa CCM.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
.gif)


0 Responses to “PINDA AZUA TENA!”
Post a Comment