Friday, February 6, 2015

PINDA AZUA TENA!




Kauli ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuwa wanafunzi walioshiriki gwaride na halaiki kwenye sherehe za miaka 38 ya CCM mjini Songea ni watoto wa wanachama wa chama hicho, imekosolewa na wananchi na wabunge ambao walifikia uamuzi wa kuomba mwongozo.

Sherehe hizo zilifanyika Jumapili ya Februari Mosi kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea, zikishirikisha makundi mbalimbali, wakiwamo wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ambao walivalia sare za CCM na kuimba nyimbo za chama hicho huku wakicheza gwaride na halaiki, ambayo kwa kawaida huchukua muda mrefu kujifunza na kuielewa.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Susan Lyimo, mtendaji huyo mkuu wa Serikali alitetea ushiriki wa watoto hao wapatao 500 kwenye sherehe hizo akisema ni sehemu ya mfumo wa wanachama wa CCM.

0 Responses to “PINDA AZUA TENA!”

Post a Comment

More to Read