Friday, July 24, 2015
UANDIKISHAJI BVR DAR WATAWALIWA NA CHANGAMOTO.
Do you like this story?
![]() |
Mwananchi aliyekwenda kujiandikisha (kulia) akiweka vidole kwenye mashine ya kuchukua alama za vidole eneo la Mlimani City, Dar. |
![]() |
Wananchi wakiwa katika foleni kusubiria kujiandikisha maeneo ya Mlimani City, Dar. |
![]() |
Hapa wananchi wakitafakari hatma yao ya kujiandikisha. |
IKIWA sasa ni siku ya tatu tangu zoezi la
uandikishaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura uanze kwa teknolojia ya
Biometric Voters Regitration (BVR), hali imezidi tete baada ya wakazi wa Dar
kupata usumbufu wa kuamka asubuhi na mapema kwenda kujiandikisha na kurudi bila
mafanikio.
Mapema hii leo mwandishi wetu amefanikiwa
kutembelea baadhi ya vituo kama vya Sinza, Shule ya Msingi Mapambano, Mwenge,
Kijitonyama pamoja na maeneo ya Mlimani City Dar na kushuhudia umati mkubwa
ukiwa kwenye foleni kwa ajili ya kujiandikisha.
Katika baadhi ya vituo hivyo, zoezi
lilionekana likiendelea vizuri huku baadhi ya maeneo yakiwa na changamoto za
wananchi kulalamikia ubovu ‘Solar power’ zinazotumika katika mitambo ya uandikishaji
kuwa jua linapopungua na mitambo husimama kutokufanya kazi.
Kituo Cha Kijitonyama-Mpakani B, maeneo ya
Mori wananchi wengi wamelalamikia foleni kuwa ndefu na zoezi kwenda taratibu,
huku wakilalamikia suala la kuandikishwa majina kisha kupatiwa vitambulisho
siku inayofuata.
“Tunaomba waandikishaji wa BVR wasilaze
majina kwa kuwa inasababisha msongamano na vurugu kwa wananchi wanaojitokeza
siku inayofuata tena wakiwa wameamka alfajiri kushinda vituoni hapo,” alisema
Amina Suleiman, mkazi wa Sinza-Mori jijini Dar.
Aidha, kwa upande wa waandikishaji nao
wamelalamikia wananchi kwa kutozingatia taarifa zinazotelewa juu ya changamoto
za kwenda kujiandikisha wakiwa wamejipaka mafuta mikononi hatua inayosababisha
mashine kutofanya kazi vizuri.
Waandikishaji hao pia wamezungumzia suala la
wananchi kutokuwa wavumilivu katika changamoto hizo wanazokutana nazo pindi
wanapokwenda kujiandikisha, hasa pale wanapotumia lugha za kuudhi na kuwataka
kuwa wavumilivu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “UANDIKISHAJI BVR DAR WATAWALIWA NA CHANGAMOTO.”
Post a Comment