Saturday, August 27, 2016
SIMBA WADINDIWA NA JKT RUVU TAIFA
Do you like this story?
![]() |
Mashabiki wa Simba wakishuhudia Mtanange huo katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Saalam(Picha na Halid Mhina wa Fahari News Dar es Salaam) |
Katika
muendelezo wa ligi kuu Vodacom Tanzania leo wekundu wa Msimbazi Simba
walikaribishwa na Jkt Ruvu katika mchezo
uliopigwa uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam.
Mchezo ambao
ulikuwa wa kwanza kwa Jkt Ruvu na wa pili kwa Simba ulimalizika kwa kutoka sare
ya bila kufungana (0-0) pale mwamuzi
Selemani Kinugani alipo puliza kipenga cha kuashiria mchezo kumalizika.
Licha ya
Simba kulishambulia sana goli la Jkt Ruvu katika kipindi cha pili lakini mikiki yao haikuvuna
kitu kwa mlinda mlango wa Jkt Ruvu Said Kipao.
Simba
wamegawana point moja moja na Jkt Ruvu
na kufanya kufikisha jumla ya Point 4 wakiwa wameshuka dimbani mara Mbili.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SIMBA WADINDIWA NA JKT RUVU TAIFA”
Post a Comment