Saturday, March 1, 2014
OMEGA SEME ARUDI TENA YANGA
Do you like this story?
MCHEZAJI WA TANZANIA PRISONS OMEGA SEME |
MCHEZAJI kiungo wa Timu ya Tanzania Prisons Omega
Seme, amesema anafurahia kurudi tena kwenye timu yake ya zamani ya
Yanga mara mzunguko wa pili wa ligi kuu utakapomalizika.
Seme, ameyasema hayo leo, wakati
akizungumza na Fahari News mara baada ya kumaliza mazoezi ya asubuhi kwenye uwanja wa timu ya Tanzania Prisons,
licha ya kushindwa kuweka wazi usajili wake huo kwa klabu ya Yanga
Africans.
Amesema, mchezaji anapochezea klabu
kubwa kama Yanga, Simba na Azam anakuwa na uwezo mkubwa na ujuzi wa
kiuchezaji tofauti na timu ndogo.
“Kweli nimekubali kurudi tena kwenye
timu yangu ya Yanga ile ni timu kubwa hivyo nitapata ujuzi zaidi kutokana
na kucheza mechi nyingi tofauti na sasa,”amesema.
Aidha, amesema licha ya kwamba
anatarajia kuondoka kwenye timu hiyo ya Tanzania Prisons mara ya
kumalizika kwa mashindano hayo ya ligi kuu lakini anamatumaini
makubwa na kikosi hicho kufanya vizuri zaidi kutokana na mikakati mizuri
ya kocha wao Mwamwaja
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “OMEGA SEME ARUDI TENA YANGA”
Post a Comment