Wednesday, April 2, 2014
AJARIBU KUJIZIKA KUKWEPA MATATIZO YA NDOA KENYA.
Do you like this story?
Mwanamume mmoja nchini Kenya
aliwaacha wakazi wa kijiji cha Tivani mkoa wa Bonde la uffa vinywa wazi baada
ya kujichimbia kaburi na hata kujaribu kujizika mwenyewe kutokana na alichosema
ni matatizo ya ndoa.
Kwa mujibu wa kituo cha runinga cha
KTN nchini Kenya, tukio hilo lililotokea Jumanne asubuhi na kuwashangaza wakazi
wa eneo la Trans Nzoia mkoa wa Rift Valley
Mwanamume huyo, alidai kuwa ana
matatizo ya ndoa ambayo yeye mwenyewe ameshidwa kuyatatua na kwa hivyo kwake
kilichosalia ni kwenda mbinguni.
Alisema mkewe alikuwa amemwambia
jambo ambalo lilimkera roho na ndhio maana akaamua kujitoa uhai.
Mwanamume huyo kwa jina Kipsang ,
alichimba kaburi hilo usiku na hata kujaribu kujizika akiwa hai wakati mkewe na
watoto wake walipokuwa wanalala.
Wanakijiji katika kijiji cha Tivani
walikuwa na wasiwasi kuwa mwanamume huyo alikuwa amerukwa na akili ingawa
walikiri kwamba yeye na mkewe wamekuwa wakikumwba na matatizo ya ndoa.
Mkewe alisema kuwa amechoshwa na
mwanamume huyo ambaye ametelekeza familia na majukumu yake.
Baba huyo wa watoto wawili ambaye ni
kondakta wa matatu, hatimaye aliondoka katika kaburi hilo baada ya wanakijiji
kumsihi huku wazee wakiwataka watu kupanda migomba ya Ndizi neneo alilokuwa
amechimba kaburi hilo ili kuzuia mikosi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “AJARIBU KUJIZIKA KUKWEPA MATATIZO YA NDOA KENYA.”
Post a Comment