Wednesday, April 9, 2014
MVUA ZASABABISHA MAUAJI YA MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU JIJINI DAR.
Do you like this story?
MVUA kubwa zinazoendelea kunyesha
jijini Dar es Salaam zimezidi kusababisha maafa ambapo jana ukuta wa hosteli za
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam zilizopo eneo la Mabibo ulianguka baada ya
kuzidiwa na maji na kusababisha kifo cha mtu mmoja.
Mwenyekiti wa Kata ya Makuburi, Moshi
Kaftany, aliliambia gazeti hili kwa simu kuwa maafa hayo yalitokea kati
ya saa 7:00 na 8:00 mchana ambapo ukuta huo uliangukia nyumba mbili za jirani
na kusababisha maafa hayo.
Alisema kuwa ndani ya nyumba moja
alikuwemo mfanyakazi wa ndani wa kike ambaye maji yalimfika kifuani na kumzidi
nguvu.
Kaftany alifafanua kuwa hadi
alipopatiwa msaada wa kutolewa ili kupelekwa hospitali alikuwa tayari
amefariki.
“Ukuta wa Mabibo ni mrefu, wapata mita
60 kwenda juu, sasa mvua ilipokuwa kubwa maji yakaongezeka kwa kasi na
kuuangusha na hatimaye kusababisha hayo mauaji,” alisema.
Kwa mujibu wa Kaftany, marehemu huyo
ambaye hakutambulika jina lake mapema, anakadiriwa kuwa na umri kati ya miaka
20 au 21.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MVUA ZASABABISHA MAUAJI YA MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU JIJINI DAR.”
Post a Comment