Wednesday, April 9, 2014
AJALI ZA BARABARANI ZAONGEZEKA KWA KASI MKOANI IRINGA.
Do you like this story?
TAKWIMU zinaonyesha kuwepo kwa ongezeko
la ajali za barabarani mara saba zaidi zinazohusisha pikipiki Mkoa wa Iringa
kati ya Januari 1 hadi Machi 31 ikilinganishwa na miezi kama hii mwaka jana.
Akizungumza na Mwandishi wa habari hii,
Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani mkoani Iringa, Leopold Fungu,
alisema ongezeko la ajali hizo linasababishwa na biashara ya pikipiki kubeba
abiria.
Alisema jumla ya ajali zote za pikipiki
kipindi hicho kwa mwaka huu ni 19 ikilinganishwa na ajali 12 za mwaka jana kwa
kipindi kama hicho.
Kuhusu vifo vinavyotokana na ajali
hizo, alisema vimeongezeka hadi kufikia 12 kwa mwaka huu
ikilinganishwa na mwaka jana ambapo vilitokea vifo 8 sawa na ongezeka la vifo
vinne kwa ajali za pikipiki.
Kamanda Fungu alisema ajali hizo
zilisababisha majeruhi ambapo kwa kipindi hicho watu saba walijeruhiwa tofauti
na mwaka jana ambapo waliojeruhiwa walikuwa watatu wakati mwaka huu walikuwa
wanne.
Aliwataka madereva wa pikipiki
kuzingatia sheria zilizowekwa ili kupunguza ajali zinazosababisha hasara kwa
familia na taifa.
Kwa mujibu wa kamanda huyo, ongezeko la
ajali hizo limesababisha polisi kuweka mikakati ya kuzipunguza kwa kipindi
kilichobaki cha mwaka 2014 ambapo ni ushiriki wa jamii na elimu kwa umma na
kwamba watapanua wigo wa kueneza elimu kwa umma.
Na Denis Mlowe, Iringa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “AJALI ZA BARABARANI ZAONGEZEKA KWA KASI MKOANI IRINGA. ”
Post a Comment