Saturday, June 14, 2014
HAUSIGELI ATESWA KUJERUHIWA NYETI ZAKE NA BOSS WAKE.
Do you like this story?
Mtoto Merina Mathayo (15) amelazwa katika Taasisi ya Tiba ya
Mifupa (Moi) Muhimbili Dar es Salaam, baada ya kuteswa na
kujeruhiwa kichwani kwa kipigo maeneo mbalimbali ya mwili na bosi wake
kwa miaka miwili.
Merina amelazwa Moi baada ya kupewa rufaa na Hospitali ya
Mwananyamala alipokuwa amelazwa awali, kutokana na majeraha hayo ambayo
yanadaiwa kusababishwa kung’atwa kwa meno na kupigwa kwa vitu mbalimbali
mara kwa mara.
Akizungumza kwa shida Merina alisema amekuwa katika hali ya
mateso tangu mwaka 2012, kwani bosi wake huyo ambaye anamtaja kuwa ni
mwanasheria mkazi wa Boko amekuwa na tabia ya kumpiga na vitu mbalimbali akiwa
amemvua nguo.
“Haya
marejaha niliyonayo sasa, alinipiga kwa fagio la chooni akamalizia na jagi,
kisha akapiga simu nyumbani kwetu huko Ishozi Kiziba mkoani Kagera, akawaambia
wazazi kwamba amenikung’uta kichwa kwa sababu mimi ni mjeuri,” alieleza Merina
na kuongeza:
“Mara
kwa mara amekuwa na tabia ya kunivua nguo na kunipiga na chochote
anachojisikia, ananing’ata kisha ananipakaza chumvi kwenye majeraha,” alisema
Merina.
“Mara
zote anazonipiga huniambia kwamba sijafanya kazi vizuri au sijamaliza
kuzifanya, lakini mwanaye ambaye ninamlea huwa analia sana
akimwambia usimpige dada, mwachie,” alisema Merina.
Alibainisha
kwamba dada wa mtuhumiwa huyo anayemtaja kwa jina la Josephine Rwechungura,
baada ya kukerwa na vitendo hivyo vya kikatili alivyotendewa ndiye alimpeleka
hospitali.
Merina
alisema kuwa hajawahi kupewa malipo yake na bosi huyo ambaye walikubaliana
mshahara wa Sh40,000 na Sh20,000 hutumwa kwa wazazi wake na zilizobaki
alikuwa anadai kwamba anamwekea.
Ofisa
Uhusiano wa Moi, Patrick Mvungi alisema wamempokea Merina juzi saa 7.00
usiku, baada ya kuelezwa historia ya majeraha yake uongozi umeguswa na
kujitolea kugharimia matibabu yake.
“Madaktari
wamesema kwamba anatakiwa kufanyiwa kipimo kikubwa cha CTS can ambacho
kitawezesha kujua majeraha aliyonayo yana ukubwa gani, gharama zake ni
Sh250,000 ambazo Moi itazitoa na kumpatia matibabu bure,” alisema Mvungi.
Awali
Katibu Afya wa Hospitali ya Mwananyamala, Edwin Bisakala alisema Merina
alipelekwa hospitalini hapo Juni 11 mwaka huu na msamaria mwema, baada ya
madaktari kumwona walibaini kwamba ana majeraha makubwa kichwani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “HAUSIGELI ATESWA KUJERUHIWA NYETI ZAKE NA BOSS WAKE.”
Post a Comment