Wednesday, June 11, 2014
KESI YA WATANZANIA WATATU DHIDI YA KESI YA, RWANDA,UGANDA YAANZA KUNGURUMA
Do you like this story?
Kesi iliyofunguliwa na
watanzania watatu ally hatibu Msangi, david
makatha na john bwenda katika mahakama
ya jumuiya ya afrika mashariki (EAC) wakiomba itoe zuio la muda kwa Kenya ,Uganda,na Rwanda
kufanya vikao bila kuzishrikisha tanzania na Burundi imeanza kunguruma.
Katika siku hiyo ya kwanza
juzi hoja na malumbano ya kikanuni vilikwamisha
shauri hilo lonalosikilizwa na
jopo la majaji watano wakiongozwa na
jaji kiongozi jean bosco butasi baada ya wakili amable malala anayemwakilisha
mwanasheria mkuu wa Rwanda kuibua hoja
ya kutopatiwa nyaraka za shauri hilo
kama kanuni za 14 na 15 za mahakama hiyo inavyoeleza.
Watanzania hao
wanaowakilishwa na wakili jimmy obedi wa dar es salaam watajibu hoja za rwanda
kabla ya juli 7 mwaka huu na baada ya hapo mahakama itapanga siku ya kusikiliza
shauri hilo linalovuta hisia za
watu wa Afrika mashariki walalamikaji hao pia waliomba mahakama
kuzizuia nchi hizo tatu kutekeleza makubaliano ya vikao vya enthebe Uganda Mombasa
Kenya na Kigali, Rwanda bila kuzishirkisha Tanzania na Burundi hadi shauri litakaposikilizwa na kuamuliwa.
Mdaiwa wa kwanza katika
shauri ni katibu mkuu wa EAC anayewakilishwa na waakili dk antony kafumbe
mwanasheria mkuu wa Kenya ambaye ni mdaiwa wa pili anawakilishwa na
mawakili wawili Emanuel bita na pete ngumi.
Mdaiwa watatu ni mwanasheria
mkuu wa Uganda anayewakilishwa na mawakili watatu Elisha bafirawala , Richard
adrole na mureen ijang’ mwanasheria wa
Rwanda ni mdaiwa wanne
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KESI YA WATANZANIA WATATU DHIDI YA KESI YA, RWANDA,UGANDA YAANZA KUNGURUMA”
Post a Comment