Wednesday, June 11, 2014
MBUNGE ASEMA MALAWI IMEANZA KUWATISHA WATANZANIA
Do you like this story?
Mzozo kati ya Tanzania na Malawi huenda ukaanza upya baada ya mbunge
wa ileje (CCM) aliko kibona kusema
bungeni kwamba ndege za Malawi zimekuwa zikiruka katika anga ya Tanzania na
kuwatisha wananchi.
Kwa kuzingatia uhusiano
uliopo kati ya Tanzania na Malawi naomba mwongozo wako maana ndege za nchi hii sasa zinaingia hadi
Tanzania na kuwatia hofu wananchi alisema kibona.
Kauli ya mbunge huyo imekuja
wakati msimamo rais wa Malawi profeser
peter mutharika kuhusu mzozo uliopo kati
ya nchi hiyo na Tanzania kuhusu ziwa nyasa ukiwekwa bayana hatakuwa na
mjadala kuhusu mpaka wan chi hizo akidai
kuwa ziwa nyasa ni la Malawi pekee.
Kibona amesema kwa takribani
wiki mbili sasa ndege hizo zimekuwa zikionekana upande wa Tanzania lakini hakuna kuli yoyote iliyotolewa na serikali hadi sasa.
Katika mwongozo wake spika
anne makinda amesema jambo hili ni umuhimu sana hivyo serikali ni lazima
ijipange ili kulijibu aidha naibu spika job ndugai aliongeza hili jambo ni zito
na serikali haiwezi kukurupuka kujibu
kwanza lazima majibu hayo yamfikie rais jakaya kikwete.
Hakuna haja ya kuendelea
kujadiliana ziwa Malawi ni mali ya Malawi
na litaendelea kuwa la Malawi daima aliwaambia wananchi hao huku
akimshutumi mtangulizi wake joyce banda kwamba alikuwa dhaifu kiasi cha kutoa
fursa kwa Tanzania kutumia udhaifu huo
kutaka kupora ziwa hilo.
Hata hivyo akizungumza
bungeni wakati akiwasilisha bajeti ya wizara yake waziri wa mambo ya nje na
ushirikiano wa kimataifa Bernard membe alisema Tanzania ilikuwa ikifuatilia kwa
karibu uchunguzi wa Malawi na kwamba iko
tayari kufanya kazi na serikali yoyote
itkayoingilia madarakani
Juhudi za usuluhisho wa
mzozo huo zinafanyika chini ya uongozi wa rais mstaafu wa msumbuji Joachim
chisano akisaidiwa na rais mstaafu wa afrika kusini thabo Mbeki
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MBUNGE ASEMA MALAWI IMEANZA KUWATISHA WATANZANIA”
Post a Comment