Friday, June 13, 2014
LORI LA MAFUTA LATEKETEA KWA MOTO BAADA YA KUGONGANA NA LORI LINGINE MBARALI MBEYA
Do you like this story?
Lori la kusafirisha mafuta likiwa na
shehena kubwa ya mafuta aina ya Diesel limeteketea kwa moto baada ya kupata
ajali ya kugongwa na lori lingine katika eneo la Igurusi wilayani Mbarali,
Mbeya.
Ajali hiyo imetokea ikihusisha
lori lenye namba za usajili T 417 ABF, mali ya kampuni ya Camel oil ambalo
lilikuwa likisafirisha lita 35,000 za mafuta aina ya diesel kutoka jijini Dar
es salaam kwenda nchini Congo DRC ambalo linadaiwa kugongwa na lori lingine.
Baadhi ya wananchi ambao wameshuhudia
ajali hiyo wameitaka serikali kuwalazimisha wamiliki wa malori
kuhakikisha magari yao yanakuwa na madereva wa akiba kwa kuwa wanaamini kuwa
ajali hiyo imesababishwa na dereva wa lori moja wapo kusinzia wakati akiendesha
gari kutokana na uchovu wa safari ndefu.
Mpaka ripota wetu anaondoka katika eneo
hilo la ajali, bado lori hilo lilikuwa likiendelea kuteketea huku kukiwa hakuna
msaada wowote wa kuuzima moto huo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “LORI LA MAFUTA LATEKETEA KWA MOTO BAADA YA KUGONGANA NA LORI LINGINE MBARALI MBEYA ”
Post a Comment