Friday, June 13, 2014
WATU WANNE WAFARIKI DUNIA KWA KUUMWA NA MBWA WENYE KICHAA WILAYANI SONGEA
Do you like this story?
Kuanzia mwezi Januari hadi Juni mwaka
huu watu wa nane wamefariki dunia kwa kuumwa na mbwa wenye kichaa katika
manispaa ya Songea.
Huku manispaa ya Songea inayotikiswa
kwa ugonjwa huo ikiwa haina dawa za kutibu watu walioumwa na mbwa kichaa na pia
idara yake ya mifugo haina pesa za mafuta kuzungukia kuua mbwa wenye kichaa.
Taarifa hiyo imetolewa na Kaimu afisa
mifugo wa manispaa ya Songea mkoani Ruvuma Bw.Gaspar Tillya na kwamba kutoka na
hali hiyo msako mkali umekuwa ukiendeshwa wa kuwasaka mbwa wenye kichaa ingawa
unakwazwa na ukosefu wa pesa huku wanajeshi wakisaidia kusaka mbwa hao
kutokana na baadhi ya mbwa hao kuingia kwenye kambi ya jeshi ya Chandamali ya
mjini Songea.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WATU WANNE WAFARIKI DUNIA KWA KUUMWA NA MBWA WENYE KICHAA WILAYANI SONGEA ”
Post a Comment